Daktari afariki na Ebola Liberia
Daktari Samuel Brisbane aliambukizwa viini vya ugonjwa huo alipokuwa akiwatibu wagonjwa wa Ebola katika mji mkuu wa Monrovia.
Alihudumu kama daktari wa watu wengi maarufu akiwemo rais wa zamani Charles Taylor.
Shirika la afya duniani WHO linasema kuwa takriban watu 660 wamethibitishwa ama wanashukiwa kufariki na ugonjwa huo Magharibi mwa Afrika tangu mwezi February na kuufanya kuwa ugonjwa m'baya zaidi tangu uzuke.