Wazazi wa binti mwenye ulemavu wa viungo na akili, Farida Abdalah (18) mkazi wa Lukobe Juu wameiomba Serikali, wasamaria wema na wadau mbalimbali kumsaidia binti yao huyo ambaye kwa sasa amelazwa katika hospitali ya rufaa na anaendelea kufanyiwa uchunguzi wa afya yake.
https://samchardtz.blogspot.com/2014/06/wazazi-wa-binti-mwenye-ulemavu-wa.html
Binti
Farida Abdalah (18) ambaye ni mlemavu wa viungo na akili akiwa amekaa
kwenye kochi nyumbani kabla ya kupelekwa Ofisi za Dawati la Jinsia la
Polisi. Picha na Hamida Shariff, Mwananchi
Wazazi wa binti mwenye ulemavu wa viungo na akili, Farida Abdalah (18)
mkazi wa Lukobe Juu wameiomba Serikali, wasamaria wema na wadau
mbalimbali kumsaidia binti yao huyo ambaye kwa sasa amelazwa katika
hospitali ya rufaa na anaendelea kufanyiwa uchunguzi wa afya yake.
Pia
wazazi hao ambao walionekana kuwa na hali ngumu ya kimaisha waliomba
msaada wa kupatiwa matibabu ya viungo na akili kwa binti yao ili aweze
kutembea na kujitambua, kwani kwa sasa binti huyo amekuwa akilala tu
kitandani.
Maisha
ya binti huyo ambaye umri wake haulingani na umbo lake yameguswa na
watu wengi, kwani amekuwa haongei, halii, hasikii na wala hajitambui
hivyo amekuwa akivalishwa nepi na kubebwa kama mtoto mchanga.