Flatnews

KESI YA PISTORIUS, BINAMU APASUA JIPU MAHAKAMANI

Mwanariadha Oscar Pistorius kesi yake kusikilizwa tena kesho.




Mwanariadha Oscar Pistorius kesi yake kusikilizwa tena kesho.
Mwanariadha Oscar Pistorius kesi yake kusikilizwa tena kesho.
Kesi inayomkabili Mwanariadha wa Afrika Kusini Oscar Pistorius imeendelea siku ya leo ambapo binamu   yake   marehemu  Reeva ameamua kupasua jipu mahakamani hapo nchini Afrika Kusini.
Aidha, Binamu huyo ambaye ni   Kim Martin ameiambia mahakama mjini Pretoria Afrika Kusini kuwa Mwanariadha Pistorius  anapaswa kupewa adhabu kali  kwa kumuua mpenzi wake Reeva Steenkamp.

Upande wa utetezi , unasema kuwa Pistorius anapaswa kupewa kifungo cha nyumbani na kuhudumia jamii kwa kosa lake , pendekzo ambalo kingozi wa mashitaka Garrie Nel ameelezea kushutushwa nalo.
Nao  Upande wa mashitaka unasisitiza Pistorius apewe kifungo jela akisema kitendo chake kimesababisha huzuni na kadhia kubwa kwa familia.
Pistorius alipatikana na kosa la mauaji bila kukusudia mwezi jana na huenda akakabiliwa na kifungo cha hadi miaka 15 jela, lakini jaji anaweza kumpa kifungo cha nje au hata kumtoza  faini.
Katika hatua nyingine Jaji, Thokozile Masipa, ameahirisha vikao vya mahakama  hiyo hadi  siku ya  Ijumaa asubuhi.

Post a Comment

emo-but-icon

item