Ukawa Wazua Hofu, Polisi Wajipanga Kuwakabiri
U moja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), umezua hofu kubwa bungeni kutokana na hali ya kutangaza msimamo wao wa kutokukubaliana ...
https://samchardtz.blogspot.com/2015/11/ukawa-wazua-hofu-polisi-wajipanga.html
Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), umezua hofu kubwa bungeni kutokana na hali ya kutangaza msimamo wao wa kutokukubaliana na Rais John Magufuli kulihutubia Bunge.
Jana
umoja huo ulitangaza rasmi kwamba umemwandikia spika barua ya kuhoji
uhalali wa Rais kulihutubua bunge wakati uchaguzi wa Zanzibar umefutwa
na kulifanya taifa la Zanzibar kutokuwa na rais.
Hali
hiyo imeifanya serikali kuwa na hofu kubwa ambayo inaonekana kuwatesa
viongozi wa CCM siku ya leo iwapo msimamo wao utaendelea kuwa huo.
Ili
kuonesha kuwa hofu ni kubwa leo kuanzia asubuhi, maeneo mbalimbali ya
mji wa Dodoma hususani katika maeneo ya bunge kulikuwepo na magari ya polisi ya maji ya kuwasha.
Mbali
na magari ya polisi yenye maji ya kuwasha yakiwa yameegeshwa katika
maeneo mbalimbali ya bunge, magari mengine ya jeshi la polisi
yalionekana kurandaranda huku yakiwa yamesheheni askari.
Hali
hiyo imetafsiriwa na baadhi ya wakazi wa mji wa Dodoma kuwa ni njia
pekee ya kuwatishia watanzania kutokana na tangazo la Ukawa la kutomtaka
Rais John Magufuli kulihutubia Bunge.