Flatnews

KIMENUKA CCM:..VURUGU KUBWA YAZUKA CCM WABUNGE HAWA WASHIKANA VIKALI KISA NI UNAIBU SPIKA

                                    Vita ya Unaibu Spika ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), imefikia patamu baada ya idadi ya wanacham...




                                   

Vita ya Unaibu Spika ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), imefikia patamu baada ya idadi ya wanachama watano kuchukua na kurejesha fomu za kuomba ridhaa ya kugombea nafasi hiyo.
Jana chama hicho kilitangaza majina ya wanachama watano walioomba nafasi hiyo na utaratibu wa kupitisha majina matatu ya wabunge wake kwa ajili ya kupitisha jina moja.
Kikao cha Kamati ya Uongozi ya Wabunge wa CCM, kitakutana na kupitisha jina la mgombea wa nafasi ya Naibu Spika, wa Bunge la 11, na baadaye majina matatu kupelekwa kwa wabunge wa chama hicho kwa ajili ya kupigiwa kura.
Hadi jana jioni wabunge watano walikuwa wamerudisha fomu za kuwania nafasi hiyo, na jana usiku kamati na wabunge wa CCM ilikutana kupitisha jina moja la mbunge atakayepambana na wagombea wa vyama vingine.
Waliochukua fomu ni Mbunge wa Ilala, Mussa Azzan Zungu; Mbunge wa kuteuliwa, Dk. Tulia Ackson; Mbunge wa Donge, Sadifa Juma Khalifa; Mbunge wa Viti Maalum, Mariam Kisangi na Bahati Ali Abeid.
Akizungumza na waandishi wa habari, Katibu wa Kamati ya Wabunge wa CCM, Jenister Mhagama, alisema kikao cha kwanza cha kuchuja majina hayo na kubakiwa na matatu ni cha Kamati ya Uongozi.
“Leo (jana) usiku kikao cha Kamati ya Uongozi ya wabunge wa CCM kitafanyika na kutoa majina matatu ambayo yatapelekwa katika kikao cha wabunge wote katika ofisi za chama, ambao watatoa jina moja la kwenda kuwania nafasi ya Naibu Spika,” alisema.
Alisema Naibu Spika anatarajiwa kuchaguliwa leo, baada ya kumalizika uchaguzi wa Spika ambao mgombea wa CCM, Job Ndugai, kushinda kwa asilimia 70 ya kura katika uchaguzi uliofanyika jana.
SAKAYA KUWAKILISHA UKAWA
Wakati CCM ikitarajia kutoa jina la mgombea Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) unaoundwa na vyama vya NCCR-Mageuzi, Chadema, NLD na CUF, wametoa jina la Mbunge wa jimbo la Kaliua, Magdalena Sakaya (CUF).
MPAMBANO
Vita katika nafasi ya Naibu Spika wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano imeanza kujitokeza, baada ya baadhi ya vigogo wa CCM, kutolikubali jina la Mbunge Mteule wa Ilala, Mussa Azzan Zungu.
Vyanzo vya uhakika kutoka ndani ya CCM ambavyo havikutaka kutajwa majina, vinaeleza kuwa wabunge wengi wa CCM wanamtaka Zungu kushika nafasi hiyo, lakini kumekuwapo na shinikizo kutoka ngazi ya juu kutaka kuondolewa jina lake.
 “Sisi tunataka Zungu, lakini tunaona dalili za wazi na jitihada za mtu kuandaliwa kushika nafasi hiyo, ni wazi kuwa watatugawa na watasababisha nafasi hiyo kwenda upinzani,” alisema Mbunge mteule mmoja ambaye hakutaka kutajwa jina.
 Alisema kiuhalisia hadi jana jina la Zungu ndilo lilikuwa linaaminika ndilo chaguo la wabunge, lakini hali ilibadilika jana asubuhi na kuwafanya wabunge kuchanganyikiwa.
 “Tunaona kila dalili za mmoja wa wagombea kuandaliwa kushika nafasi hii, ndiyo maana tunaona mambo yanakwenda haraka haraka,” alibainisha.
NDUGAI NA ZUNGU
Mwanzoni mwa wiki iliyopita Ndugai alipokweda kuchukua fomu, baada ya kuzungumza na waandishi wa habari, katibu wake aliwataka waandishi kutoka nje kwa kuwa ana mazungumzo mafupi na Zungu.
Walizungumza kwa dakika 10, ndipo Zungu alitoka na alikataa kuzungumza na waandishi wa habari na kesho yake alikwenda kuchukua fomu ya naibu spika.
 Inaelezwa kuwa chaguo cha Ndugai ni Zungu kuwa naibu wake, lakini wapo baadhi ya vogogo wa CCM wanaopinga jambo hilo na kkumtaka mgombea mmoja kucukua nafasi hiyo.
CHANZO: NIPASHE

Related

NEWS 7727063656011326011

Post a Comment

emo-but-icon

item