Breaking Newzzzz.......Polisi na Magari ya Washawasha Yatanda nje ya Viwanja vya Bunge!!!!
UMOJA wa Katiba ya Wananchi (UKAWA), umezua hofu kubwa bungeni kutokana na hali ya kutangaza msimamo wao wa kutokukubaliana na R...
https://samchardtz.blogspot.com/2015/11/breaking-newzzzzpolisi-na-magari-ya.html
UMOJA wa Katiba ya Wananchi (UKAWA), umezua hofu kubwa bungeni kutokana
na hali ya kutangaza msimamo wao wa kutokukubaliana na Rais John
Magufuli kulihutubia Bunge.
Jana umoja huo ulitangaza rasmi kwamba umemwandikia spika barua ya
kuhoji uhalali wa Rais kulihutubua bunge wakati uchaguzi wa Zanzibar
umefutwa na kulifanya taifa la Zanzibar kutokuwa na rais.
Hali hiyo imeifanya serikali kuwa na hofu kubwa ambayo inaonekana
kuwatesa viongozi wa CCM siku ya leo iwapo msimamo wao utaendelea kuwa
huo.
Ili kuonesha kuwa hofu ni kubwa leo kuanzia asubuhi, maeneo mbalimbali
ya mji wa Dodoma hususani katika maeneo ya bunge kuwepo kwa magari ya
polisi ya maji ya kuwasha.
Mbali na magari ya polisi yenye maji ya kuwasha yakiwa yameegeshwa
katika maeneo mbalimbali ya bunge, magari mengine ya jeshi la polisi
yalionekana kurandaranda huku yakiwa yamesheheni askari.
Hali hiyo imetafsiriwa na baadhi ya wakazi wa mji wa Dodoma kuwa ni njia
pekee ya kuwatishia watanzania kutokana na tangazo la Ukawa la
kutomtaka Rais John Magufuli kulihutubia Bunge.
Baadhi ya viongozi mbalimbali ambao walizungumza na MwanaHALISI Online
walieleza kwamba jeshi la polisi limekuwa likitumia nguvu nyingi
kuhakikisha wananchi wanatishiwa jambo ambalo ni usumbufu mkubwa na
kuwanyima haki ya kudai haki yao.
Mmoja wa makada wa Chama cha Mapinduzi (CCM) ambaye hakutaka jina lake
litajwe, amesema kitendo cha serikali kutumia jeshi la polisi kutumia
nguvu kubwa ni kinyume na utawala bora bora.
Naye mmoja wa viongozi wa bodaboda wa kituo cha Swaswa, Salumu Mohamed
Swaswa, amesema umefika wakati wa watanzania kuonesha hisia zao katika
kufanya maamuzi.
Mohammed, amesema ni wajibu wa wananchi kuhakikisha wanafanya maamuzi
ambayo yataonesha wazi utashi wao, jambo la kujua ni kwamba maandamano
ni haki ya msingi kwa watanzania pale wanapoona kwamba hawatendewi haki.
Amesema Waziri yeyeto ambaye angepatikana jambo pekee ni kuhakikisha
utendaji wa kazi kwa maslahi ya wananchi bila kujiangalia wenyewe.
Chanzo: Mwanahalisi online