Flatnews

Mwigulu achukua fomu ya Ubunge na kutoa vitisho kwa wagombea wa nafasi hiyo Iramba

  Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba akiwa katika usafiri wa bodaboda akiingia kwenye ofisi ya CCM Wilaya ya Iramba ikiwa ni ...



Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba akiwa katika usafiri wa bodaboda akiingia kwenye ofisi ya CCM Wilaya ya Iramba ikiwa ni moja ya staili ya kuwaomba kura wapiga kura wa jimbo la Iramba.

11698700_1881892685370090_7978881058570572577_n
Mwigulu Nchemba akiwasili Ofisi za chama cha Mapinduzi Wilaya ya Iramba,Mamia ya Wananchi walijumuika naye kumsindikiza ili awezekuchukua Fomu hiyo na hatimaye kuteuliwa na Chama cha Mapinduzi kuwa Mgombea Ubunge Wilaya ya Iramba.
SAM_0120
Mgombea ubunge kwa tiketi ya CCM akisaini kitabu cha mahudhurio baada ya kuwasili katika ofisi ya CCM wilaya ya Iramba na kushoto kwake ni mke wake mpendwa akimsindikiza kuchukua fomu ya kugombea nafasi ya kiti cha ubunge.
SAM_0128
Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba akijiandaa kumkabidhi katibu wa CCM Wilaya ya Iramba,Bwana Mathiasi Shidagisha shilingi milioni nne kwa ajili ya kuchukua fomu pamoja na mchango wa kuimarisha chama.
SAM_0129
Naibu waziri wa Fedha, Bwana Mwigulu Nchemba (wa kwanza kulia) akimkabidhi katibu wa CCM wilaya ya Iramba, Bwana Mathiasi Shidagisha shilingi milioni nne kwa ajili ya kuchukua fomu pamoja na mchango wa kuimarisha chama.
1610965_1881892598703432_1620203464844976362_n
Mwigulu Nchemba akimtambulisha Mke wake Bi.Neema Mwigulu kwa Wananchi waliofika kushuhudia Mbunge wao akichukua fomu ya kuwania Ubunge kwa mara nyingine katika Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2015.
SAM_0138
Mke wa Naibu waziri wa Fedha akiwasalimia wananchi waliofika kumpokea mume wake kuchukua fomu ya kuomba kuchaguliwa tena kugombea ubunge wa jimbo la Iramba.
Na Jumbe Ismailly,Iramba    
BAADA ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kupuliza kipyenga cha kuwaruhusu wanachama wake kuchukua fomu za kuomba kuteuliwa kugombea nafasi za ubunge na udiwani,Naibu Waziri wa Fedha,Lameck Nchemba Mwigulu ameanza kutoa vitisho kwa wagombea wengine wa nafasi hiyo.
Mwigulu ameanza kutoa vitisho hivyo baada ya kupata habari kutoka kwa wapembe wake kwamba kuna mgombea mmoja wa chama hicho aliyechukua fomu ya kugombea ubunge ametangaza kuwanunua wapambe wake ili aweze kuibuka kidedea katika kinyang’anyiro hicho.
Kwa mujibu wa Mwigulu mgombea yeyote yule aliyeandaa pesa nyingi kwa ajili ya kuwaanunua mawakala wake,vile vile anatakiwa kuandaa majibu juu ya pesa hizo nyingi amezipata wapi.
“Wengine wanasema wameandaa pesa nyingi kununua mawakala wangu,mimi niwaambie aliyeandaa pesa nyingi kunua mawakala wangu anatakiwa pia aandae majibu juu ya hizo pesa nyingi amezitoa wapi?”alihoji Mwigulu huku akishangiliwa na wananchi waliohudhuria mkutano huo.
Huku akijifananisha na hayati Moringe Sokoine,Mwigulu ambaye amewahi kushika nafasi ya Naibu katibu mkuu wa CCM Taifa,hakusita kuwatahadharisha baadhi ya wagombea wa nafasi hiyo kwamba wasidhani watu wale waliokuwa wakimwita Sokoine wa pili wanamtania,badala yake wajiandae kutoa maelezo ya kule walikozipatia pesa hizo za kuwanunua mawakala wake ili aweze kuibuka kidedea katika kinyang’anyiro hicho.
“Anadhania wale waliokuwa wananiita Sokoine wa pili walikuwa wanatania,hivyo anayesema ameandaa pesa nyingi atanunua mawakala wangu aandae pia majibu kwamba hizo pesa nyingi amezitoa wapi”alisisitiza huku akiwaangalia wananchi kwa hasira.
Aidha Mwigulu aliyeonyesha kukerwa na kauli ya mmoja wa wagombea wa nafasi hiyo,hata hivyo hakusita kutoa vitisho kwa wapinzani wake kwamba unapotangaza vita huku ukiwa kwenye nyumba ya vioo unatakiwa pia ujitathimini sana.
Huku akijiamini kuibuka na ushindi,mgombea huyo alisisitiza pia kwamba kutokana na kazi zilizofanyika wakati wa kipindi cha uongozi wake,hivyo ana uhakika wa kuibuka kidedea katika mpambano huo.
“Na taasisi zetu zinazosimamia uchaguzi zitasimamia,na taasisi zetu zinazosimamia maadili zitasimamia,lakini baada ya uchaguzi aliyeandaa pesa nyingi za kununua mawakala wangu aandae pia na majibu kwamba pesa zile amezitoa wapi”.alisisitiza Mwigulu.
Hata hivyo Naibu waziri huyo wa fedha aliweka bayana kwamba kuandaa pesa siyo tatizo bali kuandaa majibu ya mtazania maskini anayetokea eneo maskini ambako watu wanaokula mlo mmoja wamechanagia maabara hiyo pesa nyingi ikiwa haipo,lakini ya kununua mawakala wote itatoka wapi,ili watanzania waweze kufahamu inakotoka pesa hiyo isiyoweza kuchangia maendeleo na badala yake kununua mawakala.
Akimkabidhi fomu baada ya kulipa shilingi milioni nne,zikiwemo shilingi laki moja za fomu na 3,900,000/= za kuchangia chama,katibu wa CCM wilaya ya Iramba na mkurugenzi wa uchaguzi wilaya ya Iramba,Mathiasi Shidagisha alitumia fursa hiyo kuwatahadharisha wapembe wa wagombea wote kuacha lucha za kukashifiana.
“Kuanzia tarehe 20 tutaanza kazi ya kuwatembeza hawa wakubwa na nimewaambia waliokuja kuwa hatutaki kashfa wala kukashifu mwenzake…na Mh Mwigulu najua ni Mbunge wetu lakini ubunge wako sasa hivi unaanza upya tena ninaruhusu ufanyekazi kuanzia leo na tutawazungusha matawi yote 135”alifafanua Shidagisha.

Related

NEWS 2236567278487757211

Post a Comment

emo-but-icon

item