Flatnews

JKT RUVU KIBOKO YAO, WANANDINGA ZAIDI YA 600 WAJITOKEZA KUJARIBU BAHATI YAO MBELE YA MINZIRO

 


 http://www.fullshangweblog.com/wp-content/uploads/2013/10/JKT-RUVU-DUA1.jpg
Na Baraka Mpenja, Dar es salaam
WACHEZAJI zaidi ya 600 wamejitokeza kufanyiwa majaribio na kocha mkuu wa JKT Ruvu, Fredy Felix Minziro kwenye viwanja wa Mlalakuwa jijini Dar es salaam.
Ikiwa katika harakati za kujiimarisha kuelekea msimu mpya wa ligi kuu soka Tanzania bara, JKT Ruvu imealika wachezaji kutoka maneno mbalimbali ili kujaribu bahati zao katika kikosi cha kwanza na kikosi cha vijana.
Meneja wa JKT Ruvu, Kaptein John Sibaya amesema zoezi hilo lina mafanikio makubwa kwasababu wachezaji zaidi ya 600 wamejitokeza na benchi la ufundi linajitahidi kwa kila namna kuwajaribu wote.
“Kila mchezaji anacheza kuonesha uwezo wake. Kocha wetu Minziro anawaangalia na kuchagua wanaofaa katika mipango yake”. Alisema Kaptein Sibaya.
Sibaya aliongeza kuwa bado wanahitaji kuona vijana wengi wanajitokeza na mtu akisikia idadi hiyo asiogope bali afike Mlalakuwa ili kujaribu bahati ya kusajiliwa na JKT Ruvu.
Nao maafande wenzao wa Ruvu Shooting walitumia mfumo huo wa kutafuta wachezaji wapya chini ya kocha mkuu, Mkenya Thom Alex Olaba.
Wakati timu hizo zinatafuta wanandinga wapya kwa mfumo wa majaribio, Kagera Sugar wamesema kusajili kwa kufanya majaribio ya wachezaji kuna faida ndogo sana.
Kocha msaidizi wa klabu hiyo, Murage Kabange ameuambia mtandao huu kuwa siku ya majaribio kila mchezaji anajiandaa vizuri, lakini baadaye anaweza kuigharimu timu.
“Unajua unapoenda kwenye usaili unajiandaa vizuri kuwashawishi wanaokufanyia usaili. Mnaweza kumuona mchezaji anafaa na mkamsajili, lakini baadaye asiwepo katika mipango”.
“Sisi tunasajili kwa nafasi. Tunachagua wachezaji wakati ligi inaendelea na baada ya ligi kumalizika tunasajili wanaotufaa”. Aliongeza Kabange.

Post a Comment

emo-but-icon

item