Flatnews

TAZAMA KIJANA HUYU ANAVYOTESEKA

Sadick Suleiman akionyesha sehemu ya mguu wake uliokatwa.


Sadick Suleiman akionyesha sehemu ya mguu wake uliokatwa.

Akizungumza na gazeti hili mwishoni mwa wiki iliyopita akiwa Hospitali ya Ocean Road, Sadick alisema mguu wake ulikatwa kwa mara ya kwanza baada ya kuungua moto mwili mzima alipokuwa amekwenda kuvuna korosho.
Kijana mmoja Sadick Suleiman (24) (pichani), mkazi wa Gongo la Mboto jijini Dar es Salaam amesema kuwa madaktari wanataka kuukata mguu wake kwa mara ya tatu baada ya oparesheni mbili kufanyika pasipo mafanikio.“Nakumbuka nikiwa darasa la nne, nikiwa na watoto wenzangu tulikwenda kuokota korosho shambani Mtwara vijijini nilikokuwa nikiishi
na wazazi wangu, huko kuna kawaida ya watu kuandaa mashamba yao kwa kuyachoma moto.
“Sasa mimi na mwenzangu ambao tulikuwa wakubwa tukiwa hatujui nini kinachoendelea tulipanda juu ya mti kwa ajili ya kuangua korosho huku wenzetu wakiwa chini wanasubiri kuokota, tukiwa juu tukaona moto unawaka unakuja tulipokuwa lakini kabla hatujashuka chini, ukatuzingira,” alisema Sadick.

Aliongeza kuwa wenzao waliokuwa chini walifanikiwa kukimbia wao wakiwa juu ya mti, uliwakuta na kila walipojaribu kushuka ndivyo ulivyozidi wakapanda zaidi juu ya mti lakini mwisho walizidiwa na kuamua kujitosa kwenye moto ambapo yeye aliungua sehemu kubwa ya mwili na mwenzake aliungua mwili mzima ikiwa ni pamoja na kichwani

Post a Comment

emo-but-icon

item