Flatnews

‘Maximo sajili ‘Domayo’ mpya’

  Yanga imewapoteza viungo wake wawili wakabaji msimu huu Frank Domayo na Athuman Idd.


  Yanga imewapoteza viungo wake wawili wakabaji msimu huu Frank Domayo na Athuman Idd.


Dar es Salaam. Nyota wa zamani wa Yanga na Taifa Stars, Ally Yusuph ‘Tigana’ amemshauri kocha Marcio Maximo kumsajili kiungo mwenye uwezo wa Frank Domayo kipindi hiki cha usajili wa dirisha dogo.
Tigana aliliambia gazeti hili jana kuwa Yanga inahitaji kusajili kiungo mkabaji, nafasi ambayo imeonekana kupwaya tangu kuondoka kwa Domayo aliyejiunga na Azam msimu uliopita na sasa nafasi hiyo anacheza Mbuyu Twite.
“Twite alihamishwa kutoka beki na kucheza nafasi hiyo ambayo bado haimudu vizuri, hivyo kusababisha pengo la Domayo kuendelea kuonekana, kama kweli Yanga inahitaji kurejea kwa kasi, kocha Maximo akubali kusajili kiungo mkabaji kipindi hiki cha dirisha dogo,” alisema Tigana.
Alisema Maximo akubali au akatae, lakini Yanga inahitaji kuwa na mchezaji atakayeziba pengo la Domayo na kusisitiza kuwa timu hiyo itakuwa tishio endapo itasajili kiungo mkabaji mwenye kiwango atakayeisaidia timu mara ligi itakapoendelea Desemba 26.
Alisema upande wa mabeki kikosi hicho kiko vizuri sambamba na safu yake ya ushambuliaji ambayo alidai ina safu nzuri ya ushambuliaji.
“Tatizo la ushambuliaji, Yanga inakosa mtu wa kuwalisha mipira, Kiiza (Hamis), Tegete (Jeryson) na Bahanuzi (Said), ni washambuliaji wazuri, sasa hivi wanaonekana hawafanyi kazi sababu hawana mtu wa kuwapa mipira ya kufunga, lakini ni wazuri, hata na Jaja anayepewa nafasi na kocha,” alisema.
Naye mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Iddi Moshi ‘Mnyamwezi’ alisema wachezaji wengi wanaosajiliwa kwa bei mbaya kwa sasa si bora kama waliokuwa wanasajiliwa kwa bei mbaya miaka ya nyuma.
Moshi alisema: “Soka la sasa maneno na ujanja mwingi, zamani wachezaji walisajiliwa kwa ubora unaoonekana.
Tazama leo hii mchezaji anasajiliwa kwa Sh20milioni hadi Sh30 milioni, lakini kazi yake haionekani, zaidi utasikia kacheza mzunguko mmoja wa ligi (michezo 13) katangazwa kutimuliwa au kawekwa benchi.
“Wakati wa nyuma, mchezaji wa kiwango cha juu alisajiliwa  Sh3 milioni hadi 5, lakini kazi yake hauwezi kuifananisha na wachezaji wa sasa. Wengi wao sasa wanasajiliwa kisiasa bila ya kuangalia masilahi ya timu.

Post a Comment

emo-but-icon

item