UALIMU NGAZI YA CHETI WAFUTWA
http://samchardtz.blogspot.com/2014/10/ualimu-ngazi-ya-cheti-wafutwa.html
Serikali kupitia Waziri wa Elimu na Mafunzo ya ufundi, Dkt
Shukuru Kawambwa imefuta mafunzo ya ualimu ngazi ya cheti kuanzia
mwaka huu ili kuboresha kiwango cha elimu hapa nchini.
Akizungumza na Wanafunzi wa Chuo cha Ualimu Tabora Dkt Kawambwa amesema kuanzia mwaka huu serikali imeyafuta mafunzo ya ualimu ngazi ya cheti ikiwa ni mkakati maalumu wa kuboresha kiwango cha elimu hapa nchini.
Amesisitiza kuwa Walimu watakao ajiriwa kufundisha shule za msingi na sekondari watatakiwa kuwa na elimu ya kiwango cha diploma na kuendelea. Kuanzia sasa Wizara yake imejipanga kusimamia ubora wa elimu ndio maana imeamua kuanzisha utaratibu huo mpya.
Katika hatua nyingine kuanzia mwaka huu walimu ambao wataajiriwa kufundisha shule ya msingi na sekondari ni lazima wawe na elimu ya kiwango cha Diploma na wasiofikia kiwango hicho watapewa fulsa ya kujiendeleza.
Akizungumza na Wanafunzi wa Chuo cha Ualimu Tabora Dkt Kawambwa amesema kuanzia mwaka huu serikali imeyafuta mafunzo ya ualimu ngazi ya cheti ikiwa ni mkakati maalumu wa kuboresha kiwango cha elimu hapa nchini.
Amesisitiza kuwa Walimu watakao ajiriwa kufundisha shule za msingi na sekondari watatakiwa kuwa na elimu ya kiwango cha diploma na kuendelea. Kuanzia sasa Wizara yake imejipanga kusimamia ubora wa elimu ndio maana imeamua kuanzisha utaratibu huo mpya.
Katika hatua nyingine kuanzia mwaka huu walimu ambao wataajiriwa kufundisha shule ya msingi na sekondari ni lazima wawe na elimu ya kiwango cha Diploma na wasiofikia kiwango hicho watapewa fulsa ya kujiendeleza.
