KATAVI KUYASHUGHULIKIA MAGONJWA YASIYOPEWA KIPAUMBELE ?
Mkuu wa mkoa wa Katavi Dkt Rajabu Rutengwe .
http://samchardtz.blogspot.com/2014/10/katavi-kuyashughulikia-magonjwa.html
Mkoa wa Katavi kupitia mpango wa Taifa wa chanjo na wadau
mbalimbali utaendesha kampeni shirikishi ya chanjo dhidi ya Surua
Rubella, matone ya vitamin A, utoaji wa dawa za minyoo na kinga dhidi
ya magonjwa yasiyopewa kipaumbele.
Akizungumza katika mkutano wa Waandishi wa Habari Dkt Rajabu Rutengwe ameeleza kuwa katika kampeni hiyo chanjo ya surua-rubella itatolewa kwa watoto wote wenye umri kati ya miezi tisa hadi miaka mitano.
Matone ya Vitamini A yatatolewa kwa watoto wenye umri kati ya miezi sita na miaka mitano, dawa dhidi ya minyoo itatolewa kwa watoto wenye umri kati ya mwaka mmoja na miaka mitano, kinga tiba dhidi ya matende, mabusha au ngiri maji na usubi kwa wenye umri wa miaka mitano na kuendelea.
Kampeni ya Chanjo ya surua inaendeshwa ikiwa ni muendelezo wa utaratibu wa kufanya kampeni kila baada ya miaka mitatu, utaratibu huu unaotokana na ukweli kwamba baadhi ya watoto hukosa chanjo ya surua katika utaratibu wa kawaida.
Katika hatua hatua nyingine watoto 15 kati ya 100 wanaopewa chanjo ya surua hawajijengei kinga ya mwili ya dhidi ya surua, hali ambayo husababisha kutokea milipuko ya surua.
Akizungumza katika mkutano wa Waandishi wa Habari Dkt Rajabu Rutengwe ameeleza kuwa katika kampeni hiyo chanjo ya surua-rubella itatolewa kwa watoto wote wenye umri kati ya miezi tisa hadi miaka mitano.
Matone ya Vitamini A yatatolewa kwa watoto wenye umri kati ya miezi sita na miaka mitano, dawa dhidi ya minyoo itatolewa kwa watoto wenye umri kati ya mwaka mmoja na miaka mitano, kinga tiba dhidi ya matende, mabusha au ngiri maji na usubi kwa wenye umri wa miaka mitano na kuendelea.
Kampeni ya Chanjo ya surua inaendeshwa ikiwa ni muendelezo wa utaratibu wa kufanya kampeni kila baada ya miaka mitatu, utaratibu huu unaotokana na ukweli kwamba baadhi ya watoto hukosa chanjo ya surua katika utaratibu wa kawaida.
Katika hatua hatua nyingine watoto 15 kati ya 100 wanaopewa chanjo ya surua hawajijengei kinga ya mwili ya dhidi ya surua, hali ambayo husababisha kutokea milipuko ya surua.
