LIGI KUU VPL 2014/2015:- YANGA VS SIMBA TAIFA, MBEYA CITY VS AZAM NANI MBABE LEO
Hapo kesho Jumamosi October 18,2014, Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam utarindima kwa Dabi ya Kariakoo wakati Vigogo wa Soka N...
http://samchardtz.blogspot.com/2014/10/ligi-kuu-vpl-20142015-yanga-vs-simba.html
 |
Hapo
kesho Jumamosi October 18,2014, Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam
utarindima kwa Dabi ya Kariakoo wakati Vigogo wa Soka Nchini Tanzania na
Watani wa Jadi, Yanga SC na Simba SC, watakapovaana katika pambano lao
la kwanza la Ligi Kuu Vodacom kwa Msimu wa 2014/15.
Watani
hao wanatinga kwenye kimbembe hiki kinachongojewa Nchi nzima hasa kwa
vile Msimu huu kila Timu ina Benchi la Ufundi jipya kwa Yanga kuwa na
Kocha wa zamani wa Timu ya Taifa ya Tanzania kutoka Brazil Marcio
Maximo, na Simba kuongozwa na Kocha wao wa zamani Mzambia Patrick Phiri.
|
 |
Vile
vile mvuto zaidi ni ule wa kuona Wabrazil wa Yanga SC, Kiungo Andrey
Ferreira Coutinho na Geilson Santos ' Jaja' wakivaana na Simba SC
iliyomteka Straika wa Yanga, Mganda Emmanuel Okwi.
Hii
itakuwa Mechi ya 4 ya Ligi kwa kila Timu lakini Yanga SC wanaingia
wakiwa Nafasi ya 3 wakiwa na Pointi 6 wakati Simba SC wako Nafasi ya 10
wakiwa na Pointi 3.
Msimu
huu, Yanga SC walianza kwa kuchapwa 2-0 na Mtibwa Sugar huko Morogoro
na kisha kushinda Mechi mbili mfululizo dhidi ya Ruvu JKT na Prisons,
zote kwa Bao 2-1 kila moja.
Simba
SC wao hawajafungwa lakini hawajashinda hata Mechi moja katika Mechi 3
walizocheza kwa kutoka Sare na 2-2 na Coastal Union na Sare za 1-1 dhidi
ya Stand United na Polisi Morogoro.
Refa
wa mtanange huu wa Jumamosi ni Israel Nkongo ambae atasaidiwa na
Ferdinand Chacha na John Kanyenye wakati Hashim Abdallah atakuwa Refa wa
Akiba na Kamishna ni Salum Kikwamba.
Msimu
uliopita, Refa Israel Nkongo ndie aliesimamia Mechi ya Mahasimu hawa
ambapo Yanga SC waliongoza 3-0 hadi Mapumziko na Simba SC kuweza
kurudisha na kupata Sare ya 3-3.
|
 |
Nao
Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL), Azam FC
watakuwa na kibarua kigumu mbele ya Mbeya City ambao hawajafungwa hata
goli moja msimu huu wakati timu hizo zitakapovaana kwenye Uwanja wa
Kumbukumbu ya Sokoine mjini Mbeya keshokutwa.
Azam
FC ambao mpaka sasa wamecheza mechi 37 za Ligi bila kufungwa ikiwa Nane
za msimu wa 2012/13, 26 za msimu uliopita 2013/2014 na tatu za msimu
huu 2014/2015, watashuka kwenye uwanja huo wa Chama cha Mapinduzi (CCM)
wakiwa na kumbukumbu ya kuibuka na ushindi mgumu wa 2-1 dhidi ya
‘wababe’ hao, ushindi ambao uliwapa Ubingwa wa VPL Machi 23,mwaka jana
wakiwa mechi moja mkononi.
|