Flatnews

KURA YA HAPANA YAMPONZA, MWANASHERIA MPYA AAPISHWA RASMI ZANZIBAR


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.ALi Mohamed Shein akimuapisha  Said Hassan Said kuwa Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar katika hafla iliyofanyika leo Ikulu Mjini Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.ALi Mohamed Shein akimuapisha Said Hassan Said kuwa Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar katika hafla iliyofanyika leo Ikulu Mjini Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na  Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein Leo amemuapisha Said Hassan Said kuwa  Mwanasheria  Mkuu  wa Zanzibar katika hafla iliyofanyika Ikulu mjini Zanzibar.
Mwanasheria  huyo ameteuliwa na Rais   chini ya kifungu cha sheria  namba 55 (1) cha katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984. Uteuzi huo umefanyika oktoba  7 mwaka 2014 ambapo Bw. Hassan Said alikuwa Naibu Mwanasherian Mkuu wa serikali ya Mapinduzi Zanzibar.
Katika hatua nyingine  Bw Hassan Said anachukua nafasi ya aliyekuwa mwanasheria mkuu wa Zanziba Bw Othman Masoud ambaye uteuzi wake umefutwa kwa mujibu wa vifungu vya 53, 54(1) na 55 (3) vya katiba ya  ya Zanzibar ya mwaka 1984 na kifungu 12(3) cha sheria ya utumishi wa umma Namba 2 ya 2011.
Kufutwa  kazi  mwanasheria mkuu wa Zanzibar  kunatokana na kupiga kura ya hapana katika vifungu mbalimbali vya   katiba   iliyopendekezwa  Bungeni mjini Dodoma wiki kadhaa zilizopita.

Post a Comment

emo-but-icon

item