Malima akata makali posho za wajumbe watoro bungeni
http://samchardtz.blogspot.com/2014/08/malima-akata-makali-posho-za-wajumbe.html
Naibu Waziri wa Fedha, Adam Malima
Hatua hiyo, imeelezwa pia na mwenyekiti wa Bunge
hilo, Samuel Sitta wakati akitoa matangazo kuwa wajumbe wasiohudhuria
vikao, hawatalipwa posho zao.
Dar es Salaam. Naibu Waziri wa Fedha, Adam
Malima amesema kuna baadhi ya wajumbe wa Bunge la Katiba walioko nje,
wamekuwa wakijipitisha “pembezoni mwa ukuta wa Bunge na wengine kupiga
mluzi kutaka marafiki zao wawaandike majina” ili wapate posho.
Malima alisema juzi kuwa “wajumbe wa Bunge Maalumu
la Katiba, watapata posho zao watakapojiandikisha na kukaa bungeni,
lakini si kwa mtu kupita pembeni mwa ukuta au kupiga muluzi ili
aandikwe, hapo hatutatoa posho.
“Fedha za kila mjumbe zipo, kila atakayehudhuria
kikao ndani ya Bunge atapata fedha stahiki, lakini hatuwezi kutoa fedha
kwa mtu yeyote asiyehudhuria mkutano wala kujiandikisha...ninajua wapo
watu wanapitapita pembeni huko, waje humu ndani.”
Hatua hiyo, imeelezwa pia na mwenyekiti wa Bunge
hilo, Samuel Sitta wakati akitoa matangazo kuwa wajumbe wasiohudhuria
vikao, hawatalipwa posho zao.
Sitta alisema kuwa kanuni zimeongezwa nguvu kwa
wajumbe hasa katika suala posho na hazitapatikana kwa yeyote
asiyehudhuria vikao vya Bunge.
Katika kikao cha juzi, wajumbe wengi walitaka
wenzao ambao hawahudhurii vikao wachukuloiwe hatua na mwenyekiti na pia
wanyimwe posho zao.