AZAM FC VS MTIBWA SUGAR HAPATOSHI TAMASHA LA USIKU WA MATUMAINI TAIFA DAR
http://samchardtz.blogspot.com/2014/08/azam-fc-vs-mtibwa-sugar-hapatoshi.html
KIKOSI cha pili cha mabingwa wa ligi kuu soka
Tanzania bara, Azam fc kitakabiliana na Mtibwa Sugar katika mchezo wa kirafiki
utakaopigwa leo katika Tamasha la Usiku wa Matumaini , uwanja wa Taifa jijini
Dar es salaam.
Hii itakuwa mechi nzuri kwa timu zote kuangalia uwezo
wa wachezaji waliowasajili na wale waliopandishwa kutoka timu za vijana.
Afisa habari wa Azam fc, Jafar Idd Maganga alisema
wanauchukulia mchezo huo kwa uzito wa hali ya juu kwasababu ni nafasi nzuri kwa
wachezaji wao kuonesha uwezo mbele ya timu bora ya Mtibwa Sugar.
“Ni kweli tutakuwa na mechi na Mtibwa Sugar. Hii
ni timu nzuri yenye uzoefu mkubwa, hivyo naamini mchezo utakuwa ni mzuri.
Tumejiandaa vya kutosha na tupo tayari kwa ajili ya mechi hiyo”. Alisema Jafar.
Pia Jafar alisema baada ya mechi hiyo, wachezaji
wote watasafiri kuelekea nchini Rwanda ambapo Azam fc inashiriki michuano ya
kombe la Kagame inayoanza kutimua vumbi leo Agosti 8.
Aliongeza kuwa vikosi vyote vya Azam, A na B, vitakuwa mjini Kigali kwa ajili
ya kombe la Kagame na ligi kuu. Kikosi cha wachezaji 20 tayari kipo Kigali na
leo hii jioni kinaanza kampeni ya Kagame dhidi ya wenyeji Rayon Sport ya
Rwanda.
Kwa upande wa Mtibwa Sugar wao wamesema
wamejiandaa vizuri na watatumia fursa ya leo kuonesha wachezaji wapya
waliowasijili kwa ajili ya msimu wa 2014/2015 wa ligi kuu soka Tanzania bara.
Kocha mkuu wa klabu hiyo, Mecky Mexime amesema
Azam ni timu bora, hivyo watapata changamoto nzuri ya kupambana nao.

“Tupo salama kabisa kwa ajili ya mchezo wa kesho.
Safari hii tumechukua wachezaji kutoka ligi daraja la kwanza na michuano ya
ligi kuu, hivyo watanzania waje kuwaona.” Alisema Mexime.
“Nawaheshimu Azam fc, ni timu nzuri, lakini Mtibwa
ni wazuri pia. Kwahiyo tutaonesha mchezo mzuri.”
Mbali na mechi hii kubwa, mechi nyingine kwa
upande wa soka zitakuwa ni wabunge
mashabiki wa Simba na wale wenzao wa Yanga, Bongo Fleva dhidi ya Bongo Movie na
wengine wengi.
Pia kutakuwa na mapambo ya ngumi ambapo mapambano
ya kawaida ni baina ya msanii wa Bongo Movie, Jacob Steven (JB) na Cloud 112,
Said Memba na Khalid Chokaraa, lakini funga kazi ni baina ya Mada Maugo na
Thomas Mashali.
Burudani mbalimbali za muziki kutoka kwa wasanii
wa bongo Fleva akiwem Ali Kiba, Shilole na wengine zitakuwepo.
CHANZO NI MPENJA BLOG
