Wambura awatolea nje Friends of Simba
http://samchardtz.blogspot.com/2014/06/wambura-awatolea-nje-friends-of-simba.html
- Kauli hiyo ya Wambura ni kama inalilenga moja kwa moja kundi la Friends of Simba linaloundwa na matajiri ambao wamekuwa wafadhili wa klabu hiyo kwa muda mrefu sasa.
Kauli hiyo ya Wambura ni kama inalilenga moja kwa
moja kundi la Friends of Simba linaloundwa na matajiri ambao wamekuwa
wafadhili wa klabu hiyo kwa muda mrefu sasa.
Awali Wambura alienguliwa katika mchakato huo wa
uchaguzi utakaofanyika Juni 29 kabla ya kukata rufaa kwenye Kamati ya
Rufaa ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) na kurejeshwa aliposhinda
rufaa hiyo.
Wambura alienguliwa baada ya kuwekewa pingamizi na
baadhi ya wanachama kwa madai alisimamishwa uanachama mwaka 2010 baada
ya kupeleka masuala ya soka mahakamani kitendo ambacho ni kinyume na
taratibu za soka.
Akizungumza katika makao makuu ya Simba jana
Alhamisi, Wambura alisema: “Wafadhili hawabanwi na sheria, wanafanya kwa
wakati wanaojisikia hivyo ni ngumu kuendesha timu kwa njia hii. Pia ni
ngumu kuendesha timu kwa kutegemea kitu kimoja kwa sababu klabu ni
taasisi, hivyo lazima iwe na wadhamini wanaotoa udhamini wao kwa
makubaliano ya mkataba.”
Kwa upande mwingine, Katibu huyo wa zamani wa
Simba, alisema kitendo kilichofanywa na klabu hiyo katika uongozi
uliopita cha kuuza wachezaji tegemeo tena kwa mkopo katikati ya msimu,
ni cha kushangaza kutokana na uwezo wa wachezaji wenyewe.
Simba iliwauza Emmanuel Okwi na Shomari Kapombe mwaka jana bila kuambulia hata senti tano ikisubiri malipo hayo kufanywa sasa.
“Huwezi kuuza wachezaji wakati ligi inaendelea, ni
sawa na kuuza silaha wakati uko vitani, kamwe huwezi kushinda kwa njia
hii. Nawashangaa sana waliofanya hivyo, halafu sasa wanajitokeza na
kusema tunataka kulipwa na huyu mara hatutaki kulipwa na yule,” alisema
Wambura.
