MPYA! INAPAKULIWA.
http://samchardtz.blogspot.com/2014/06/mpya-inapakuliwa.html
Safari ya Beatrice imekaribia kuiva mara
baada ya kuchohcewa na”WEWE SI WAKAWAIDA”, Nyimbo mpya kabisa
iliyotolewa na mwimbaji Beatrice William inayobeba jina la album yake
ya kwanza, ya injili, inayotarajiwa kuzinduliwa mwezi wa nane mwaka huu.
Nyimbo hii imekuwa kivutio kikubwa na kuwapa shauku wapenzi wa muziki
wa injiri kuisubiri kwa hamu album hiyo mpya.
Beatrice ambaye awali alikuwa kivutio
kikubwa katika muziki wa bongo flava hasa baada ya kutamba katika
shindano la Bongo Star Search mwaka 2009, aliokoka na kumrudia BWANA
mwaka 2012 na kuanza kuimba nyimbo za Injiri.
Tangu alipoaanza kuimba nyimbo za injili,
Beatrice amekuwa kivutio kikubwa kwenye matamasha kwa staili yake
tofauti ya uimbaji na ushambulizi wa jukwaa, hali ambaoyo imewafanya
watu waisubiri kwa hamu album yake hii.
Kwa kuwa Bwana ameamua kukifanya chombo
hiki kipya katika kazi yake, tunaamini album hii itakuwa ni injili tosha
kwa wote watakao ipokea.
