BIBLIA YATUMIKA KUTAKA KUHALALISHA BANGI
Jani la mmea wa bangi. ©Greens Man Page
http://samchardtz.blogspot.com/2014/06/biblia-yatumika-kutaka-kuhalalisha-bangi.html
![]() |
| Jani la mmea wa bangi. ©Greens Man Page |
Wakati siku ya Jumapili ikikutanisha watu wengi kwenye nyumba za ibada,
hali imekuwa tofauti kwa seneta Constance Johnson wa jimbo la Oklahoma
huko Marekani, pale ambapo amenukuu kifungu cha Biblia kutoka kitabu cha
Mwanzo 1:29, akisema kwamba Mungu aliweka kila kitu kitumike na
binadamu, hivyo ataendesha kampeni nchini humo ili mmea wa bangi
uhalalishwe rasmi kwa matumizi ya binadamu.
"Mungu ameumba jani hili la kipekee na la maajabu, na sote tunajua
kwamba limekuwa likidharauliwa kwa kipindi cha miaka 100 iliyopita"
Seneta huyo kutoka kambi ya Democrats ananukuliwa akisema, "Ni muda
muafaka sasa wa kubadili hali hiyo hapa Oklahoma" anamalizaia kusema
seneta huyo akiwa sanjari na wakili David Slane.
Kitabu cha Mwanzo 1:29 kinaeleza; "Mungu akasema, Tazama nimewapa
kila mche utoao mbegu ulio juu ya uso wa nchi yote pia, na kila mti,
ambao matunda yake yana mbegu; vitakuwa ndivyo chakula chenu;"
Na hapa ndipo msingi wa Seneta huyo kuanza kukusanya sahihi za watu
jimboni humo ili waweze kufikia 160,000 ndani y miezi mitatu kutoka kwa
watu waliosajiliwa kupiga kura ilikuanza kupata uhalali.
Tunajua kuna watu wana chuki nasi, na wengine hata wanatumabia twende
motoni (go to hell), lakini sisi hatujali, tunataka sauti ya watu
isikike licha ya vikwazo vingi ama licha ya watunga sera wanavyoona
mambo, anamalizia kueleza Seneta huyo kwa wananchi.
Muswada ambao seneta huyo atakuwa anasainisha watu unataka kwamba, gramu
28 za bangi zitumike kwa matumizi binafsi (starehe), huku gram 85
ziidhinishwe kutumika kwenye mahospitali.
