Flatnews

KADA WA CHADEMA MAREHEMU GERVAS KALOLO KUZIKWA LEO


kakakakak_d071d.jpg

mchangaji_6682b.jpg
Mbunge wa Iringa mjini Mchungaji Peter Msigwa (Chadema) (katikati) akiwa na baadhi ya waombolezaji nyumbani kwa marehemu katika mtaa wa mashine tatu mjini Iringa, mkoani Iringa leo mchana. (Picha na Friday Simbaya)
baba_mdogo_kalolo_2c25a.jpg
Baba mdogo wa marehemu Gervas Kalolo, Mzee Raphael Kalolo (katikati) akitoa maelezo mfupi ya marehemu kwa kwa mwandishi wa mjengwablog.com nyumbani kwa marehemu katika mtaa wa mashine tatu mjini Iringa, mkoani iringa leo mchana. (Picha na Friday Simbaya)

baadhi_ya_waombelezaji_5aee6.jpg
mtaa_54e92.jpg
baadhi_ya_waombelezaji6_9328d.jpg
mmuauuau_e5de5.jpg
Katibu wa Wilaya ya Iringa-Chadema, Suzana Mgonukulima (kulia) akitoa utaratibu wa chama nyumbani kwa marehemu katika mtaa wa mashine tatu mjini Iringa, mkoani iringa leo mchana. (Picha na Friday Simbaya)
KALOLO6_6cf10.jpg


1.                WASIFU WA MAREHEMU   KUZALIWA
Marehemu GERVAS  JOHN KALOLO alizaliwa tarehe 09.11.1964 katika Hospitali ya mkoa wa Iringa

2.      ELIMU
Marehemu GERVAS  JOHN KALOLO  alisoma shule ya awali na msingi katika shule ya msingi CHEM CHEM  hapa iringa mjini na kuhitimu mwaka 1980 na baadae aliendelea na masomo ya Sekondari katika shule ya Sekondari HIGHLANDS  na kuhitimu kidato cha nne mwaka 1983.

3.      AJIRA
Mnamo mwaka 1985 marehemu aliajiriwa katika kampuni ya IMAC ambako alifanya kazi kwa muda mfupi. Na baadae aliacha kazi  na kuamua kujishughulisha na shughuli binafsi za Ujasiriamali na pia aliingia rasmi katika shughuli za kisiasa.

4.      UONGOZI KATIKA SIASA
Baada ya kuingia katika siasa mnamo mwaka 2000 alichaguliwa kuwa Mwenyekiti  wa mtaa.Na ilipofika mwaka 2005 alichaguliwa kuwa Mheshimiwa Diwani kupitia tiketi ya  Chama Cha Mapinduzi (CCM) mpaka mwaka 2010. Mwaka huo huo 2010 aliamua kujiunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na mpaka umauti unamkuta  alikuwa  mmoja wa viongozi wa CHADEMA hapa Iringa.
5.      UONGOZI KATIKA KANISA
Marehemu GERVAS KALOLO alikuwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Mtakatifu Joseph Mfanyakazi Miyomboni Parokia ya Consolata – Mshindo.

Post a Comment

emo-but-icon

item