Umoja wa Ulaya Waiasa Tanzania Kuhakikisha Sheria ya Uhalifu wa Mtandaoni ya mwaka 2015 Haikiuki Haki za Raia Wake.
Mkuu wa Umoja wa Ulaya, Mabalozi wa Ubelgiji, Denmark, Ufini, Ufaransa, Ujerumani, Ireland, Italia, Uholanzi, Hispania, Sweden, ...
https://samchardtz.blogspot.com/2015/11/umoja-wa-ulaya-waiasa-tanzania.html
Mkuu wa Umoja wa Ulaya, Mabalozi wa Ubelgiji, Denmark, Ufini, Ufaransa, Ujerumani, Ireland, Italia, Uholanzi, Hispania, Sweden, Uingereza
na Mabalozi wa Canada, Norway, Uswisi na
Marekani
Mabalozi wa Umoja wa Ulaya, Ubelgiji, Denmark, Ufini, Ufaransa, Ujerumani,
Ireland, Italia, Uholanzi, Hispania, Sweden, Uingereza na Mabalozi wa Canada,
Norway, Uswisi na Marekani
wanaikumbusha Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kuwa ilijizatiti
kutumia Sheria ya Uhalifu wa Kimtandao ya 2015 kwa namna ambayo inaheshimu
uhuru wa kimsingi na kushughulikia uwezekano wa tafsiri hasi ya sheria hiyo.
Hata hivyo, kesi za kwanza za matumizi ya sheria hiyo zimeongeza wasiwasi katika ukiukwaji wa
misingi ya uhuru.
Mabalozi wana wasiwasi kuhusu kukamatwa hivi karibuni kwa wafanyakazi wa
Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (Legal and Human Rights Centre) pamoja na
vifaa muhimu vya kiufundi, Sehemu ya 16 ya Sheria ya Uhalifu wa mitandao
ikitumika kama rejea. Matukio hayo yalitokea wakati shirika hilo lilikuwa likiandaa
maoni yaliyotolewa na waangalizi wa uchaguzi nchini kote, kazi ambayo kituo
hicho cha haki za binadamu kilipewa kibali na Tume ya Taifa ya Uchaguzi.
Mabalozi wanafahamu kuwa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu ni mwanachama wa
Umoja wa Watetezi wa Haki za Binadamu.
Kama ilivyoelekezwa katika Mkataba wa Demokrasia wa Afrika, Uchaguzi na
Utawala, Mabalozi wanaamini "kuna haja ya kuimarisha waangalizi wa
uchaguzi katika nafasi yao, hasa kwa kuzingatia umuhimu wao katika kuhakiki
utaratibu, uwazi na uaminifu wa chaguzi."
<<<<<<SOMA ZAIDI HAPA>>>>>>>