UKAWA WAMTOLEA NJE MAGUFULI NA URAIS WAKE,MBOWE APIGILIA MSUMARI WA MWISHO,SOMA HAPO KUJUA
UMOJA wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) umetangaza kususia sherehe za kuapishwa Rais Mteule, John Magufuli kwa sababu ya kutokubaliana n...
https://samchardtz.blogspot.com/2015/11/ukawa-wamtolea-nje-magufuli-na-urais.html
UMOJA wa Katiba
ya Wananchi (Ukawa) umetangaza kususia sherehe za kuapishwa Rais Mteule, John
Magufuli kwa sababu ya kutokubaliana na ushindi wake. Anaandika Erasto Masalu … (endelea).
Kwa mujimu wa taarifa iliyotolewa na Msemaji
wa Chadema, Tumaini Makene, imeeleza kuwa Ukawa hawatahudhuria tukio hilo wala
sherehe zake, huku wakiwaita wabunge wote wa Ukawa kukutaja jijini Dar es
Salaam kesho.
Ifuatayo ni taarifa iliyotolewa na Ukawa.
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ambaye
pia ni Mwenyekiti Mwenza wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), Freeman Mbowe
amesema kuwa hawatashiriki shughuli ya kuapishwa kwa Dk. John Pombe Magufuli
inayotarajiwa kufanyika Alhamis, Novemba 5, 2015.
Kauli hiyo ya Mwenyekiti Mbowe aliyoitoa leo, imekuja wakati
kukiwa bado kuna sintofahamu kubwa miongoni mwa Watanzania kuhusu mchakato wa
uchaguzi hususan upigaji kura, ukusanyaji na ujumlishaji wa matokeo
ulivyofanyika hasa katika nafasi ya urais.
“Hatutahudhuria shughuli hiyo ya kumwapisha Magufuli.
Tumekubaliana wote kwenye Ukawa, ndani ya Chadema, viongozi wetu, wabunge wetu
wote hawatahudhuria uapishwaji wala sherehe.
“Tumetoa wito kwa wananchi wote, Watanzania wote, wapenda
mabadiliko na wapenda haki wote kwa ujumla kutohudhuria shughuli hiyo,” amesema
Mwenyekiti Mbowe.
Mwenyekiti Mbowe amesisitiza kuwa Ukawa, wapenda mabadiliko wote
na Watanzania wapenda haki hawakubaliani na wanapinga mchakato wa uchaguzi
hususan matokeo ya urais ambayo, kwa mujibu wa Katiba ya Nchi aliyosema ni
mbovu, yakishatangazwa hakuna haki ya kuyapinga katika mahakama yoyote ile.
“Tunataka nchi na dunia nzima ijue wazi kuwa hatukubaliani na
mchakato wa uchaguzi hasa matokeo ya urais ambayo kwa mujibu wa Katiba yetu
mbovu, Mwenyekiti wa Tume akishatangaza hakuna mahali pa kuyapinga.”
“Matokeo ya ubunge au udiwani yanaweza kupingwa mahakamani,
lakini kwa matokeo ya urais Katiba yetu mbovu inawafunga mikono na miguu
Watanzania wote ambao wangependa waone haki imetendeka katika nafasi hiyo,”
amesema Mwenyekiti Mbowe.
“Watawala wamechezea haki ya Watanzania kupiga kura. Kura
zimehesabiwa kama karatasi za kawaida tu. Hujuma dhidi ya matokeo ya wagombea
wetu imehujumiwa waziwazi. Safari hii hujuma hazikuwa kificho tena. Kila mtu
amejionea matokeo yaliyokuwa na Jaji Lubuva si yale ambaye yalikuwa
yamebandikwa vituoni.
Hayakuwa na uhalisia na matokeo yaliyokusanywa na mawakala.
Uchaguzi umefanywa kama ni jambo lisilokuwa na maana yoyote. Hiyo ni hatari
sana kwa taifa lolote linalotaka kukuza demokrasia kama mojawapo ya nguzo za
maendeleo. Hatuwezi kukubali kufika huko,” amesema Mbowe.
Aidha, Mwenyekiti Mbowe ameongeza kusema kuwa vyama vinavyounda
Ukawa vimeitisha kikao cha Wabunge wateule wote wa vyama hivyo ambao watakutana
Alhamisi, saa 4 asubuhi, jijini Dar es Salaam.