MGOGORO ZANZIBAR!..HAPATOSHI VIGOGO WENGINE 9 WAJIUZULU>>>>SOMA HAPA
Mawaziri sita wajiuzulu kutoka katika Chama cha upinzani CUF, mawaziri hao wamechukua hatua hiyo kutokana ...
https://samchardtz.blogspot.com/2015/11/mgogoro-zanzibarhapatoshi-vigogo.html
Mawaziri sita wajiuzulu kutoka katika
Chama cha upinzani CUF, mawaziri hao wamechukua hatua hiyo kutokana na
msuguano wa kisiasa visiwani humo.
Waziri wa sheria na katiba Abubakar
Khamis Bakary alitoa kauli hiyo wakati akijibu maswali ya waandishi wa
habari juu ya maazimio yaliyofikiwa na baraza la chama la Halmashauri
kuu ya Taifa.
Mawaziri wengine waliojiuzulu ni Fatma
Abdulhabibu Fereji,Waziri wa Nchi ofisi ya Makamu wa Rais wa kwanza,
waziri wa Biashara, Viwanda na Makoso Nassor Ahmed Mazrui, Waziri wa
Miundombinu na Mawasiliano Juma Duni Haji, Waziri wa afya Rashidi
Suleiman na Waziri wa Uvuvi na Mifugo Abdillah Jihadi.
Na wengine ni, Haji Mwandani Makame
aliyekuwa Naibu Waziri wa Ardhi na Nyumba, Maji na Nishati, Naibu waziri
wa Elimu na Mafunzo Zahara Ali Hamed na Naibu Waziri wa Kilimo
Maliasili Mtumwa Kheir Mbarak.
Kwa mujibu wa Abubakary kila Waziri na
Manaibu wao wamekabidhi magari ya serikali na vifaa vingine kwa mamlaka
na kwa mujibu wa kifungu cha sheria cha (28) ya katiba ya Zanzibar,
umiliki wa ofisi kwa ajili ya wote akiwemo na Rais Dr Ali Mohamed Shein
na mawaziri kumalizika Novemba 2.