Lowassa Kuzungumza na Watanzania Kuhusu Uchaguzi Zanzibar na Msimamo wake Baada ya Magufuli Kutangazwa Mshindi
Aliyekuwa mgombea urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Edward Lowassa, ameibuka na mambo mengi mazito kuhusia...
https://samchardtz.blogspot.com/2015/11/lowassa-kuzungumza-na-watanzania-kuhusu.html
Aliyekuwa mgombea urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Edward Lowassa, ameibuka na mambo mengi mazito kuhusiana na kile kilichotokea katika uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 25 na kumuweka madarakani Rais wa Awamu ya Tano, Dk. John Magufuli.
Taarifa
kutoka ndani ya muungano wa vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya
Wananchi (Ukawa) ambavyo Lowassa alikuwa akiviwakilisha kwa nafasi ya
urais vya Chadema, Chama cha Wananchi (CUF), NCCR-Mageuzi na NLD,
inaeleza kuwa Lowassa atafichua kila kitu kuhusiana na uchaguzi huo
wakati atakapozungumza jijini Dar es Salaam leo na vyombo vya habari
vya ndani na vya kimataifa.
Kadhalika,
taarifa hiyo inaeleza kuwa mbali na kufichua mazito kuhusiana na
uchaguzi mkuu ambao yeye alitangazwa kuwa mshindi wa pili bada ya kupata
asilimia 39.97 ya kura halali zilizopigwa na kuachwa na Dk. Magufuli wa
Chama Cha Mapinduzi (CCM) aliyepata asilimia 58.46, Lowassa pia
atashirikiana na viongozi wa Ukawa kuelezea msimamo wao kuhusu uchaguzi
uliofutwa wa Zanzibar ambao mgombea urais wa CUF na Ukawa, Maalim Seif
Sharif Hamad, anadaiwa alikuwa akielekea kushinda.
Mwenyekiti
wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), Jecha Salim Jecha, ndiye aliyeufuta
uchaguzi wa Zanzibar siku tatu baada ya kufanyika kwake kutokana na
kile alichoeleza kuwa ni kuwapo kwa kasoro nyingi zilizoufanya uchaguzi
huo usiwe ‘huru na wa haki’.
Akizungumza na mtandao huu kwa
njia ya simu jana, Msemaji wa Lowassa, Aboubakar Liongo, alisema
Lowassa atazungumza leo jijini Dar es Salaam na kueleza mengi kuhusiana
na kilichotokea katika uchaguzi mkuu, akiwa pamoja na viongozi wengine
wa Ukawa akiwamo Maalim Seif.
“Lowassa
atazungumza katika mkutano huo… pia Maalim Seif anatarajiwa kuwapo.
Atazungumzia msimamo wa Ukawa juu ya hali ya Zanzibar na kutoa kauli
nini kinafuata baada ya kuporwa ushindi,” ilisema sehemu ya taarifa iliyotolewa na Liongo jana.
Aidha,
akizungumza jana, Makamu Mwenyekiti wa Chadema, Profesa Abdallah
Safari, aliwaambia wananchi kwenye mkutano wa kampeni wa kumnadi mgombea
ubunge wa chama chao jijini Arusha, Godbless Lema, kuwa Lowassa ana
mengi mazito kuhusiana na uchaguzi mkuu ambayo atayatoa leo mbele ya
waandishi wa habari wa ndani na wa kimataifa.
Aliyasema hayo kwenye viwanja vya Shule ya Msingi Ngarenaro.
Aliyasema hayo kwenye viwanja vya Shule ya Msingi Ngarenaro.
Alisema
tofauti na walivyopanga awali kuwa Lowassa ahudhuhurie mkutano huo wa
kampeni kwa ajili ya uchaguzi wa Jimbo la Arusha Mjini, sasa atafanya
hivyo wakati wa kufunga kampeni kwani jana hiyo alikuwa katika
maandalizi ya kuzungumza na waandishi, hasa kuhusiana na hujuma
zilizofanyika katika uchaguzi mkuu uliopita.
“Mnaelewa jinsi kura zake zilivyoibiwa… sasa kesho (leo) atazungumza na waandishi wa habari wa ndani na nje kuhusu kadhia hiyo,” alisema Profesa Safari na kuongeza: “Sasa atakuja siku ya mwisho ya kufunga kampeni kumnadi Lema.”
Kuhusu Zanzibar
Kwa
upande wake, Kaimu Mwenyekiti wa CUF, Twaha Taslima, ambaye pia ni
Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki, alisema kufutwa kwa uchaguzi wa
Zanzibar ni suala ambalo limewashitua wengi wengi nchini na duniani
kwani ni kukiukwa wazi wazi kwa misingi ya demokrasia.
“Uchaguzi mpya Zanzibar siyo sawa… na kila mtu anaona hiyo si sawa, lakini tunashangaa kuona uchaguzi unarudiwa. Viongozi wetu wapo na watawaambia cha kufanya,” alisema Taslima.
“Hali
inayoendelea Zanzibar inatia doa sura ya Tanzania katika uso wa Dunia.
Mimi ni mmoja wa viongozi hao, tunajiandaa kutoa tamko kesho (leo),” aliongeza
Taslima, akikumbushia uchaguzi uliofutwa Zanzibar ambao mgombea wa CUF
na Ukawa, Maalim Seif, aliwaambia waandishi wa habari kabla ya kufutwa
kwa uchaguzi huo kwamba alikuwa akiongoza kwa asilimia 52.87 kutokana na
karatasi za matokeo walizokusanya kutoka katika vituo vyote vya
uchaguzi visiwani Zanzibar.
Mwenyekiti
wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia, alisema ukimya wa Watanzania usiwafanye
watwala kuamini kuwa wao (Ukawa) ni ‘wapumbavu na malofa’ kama
alivyowatuhumus Rais mstaafu wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa, wakati wa
kampeni za uchaguzi na badala yake wanatakiwa kuzingtia sheria na
kutenda haki.