BREAKING NEWS:...HANDENI HAPATOSHI CCM YAMPITISHA MTOTO WA KIGODA KUGOMBEA JIMBO LA HANDENI MJINI
Handeni. Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM Jimbo la Handeni Mjini wamempigia kura na kumchagua tena mgombea a...
https://samchardtz.blogspot.com/2015/11/breaking-newshandeni-hapatoshi-ccm.html
Handeni. Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM Jimbo la
Handeni Mjini wamempigia kura na kumchagua tena mgombea ambae alishinda
awali Omari Abdallah Kigoda katika uchaguzi uliofanyika wilayani humo
leo baada ya kamati kuu ya CCM Taifa kutaka urudiwe.
Akitangaza matokeo hayo Mwenyekiti aliyesimamia uchaguzi huo Dk Maua
Daftari alisema kuwa wajumbe wote kwenye mkutano walikuwa 690 na
waliopiga kura ni 660 na uchaguzi ulikuwa wa wazi na haki na hakukuwa na
tatizo lolote.
Alisema Omari Kigoda amepata kura 402 na mgombea mwenzake Hamisi Mnondwa
alipata kura 257 huku kura moja ikiharibika na kufanya jumla ya kura
zote kuwa ni 660 hivyo kumtangaza Omari kuwa mshindi katika kura halali
259.
Awali kabla ya uchaguzi huo mjumbe wa kamati kuu ya chama hicho Taifa
Abdallah Bulembo alisema kuwa sababu kubwa ya kurudiwa uchaguzi huo ni
kutokana na mshindi wa kwanza na aliyemfuatia kushindwa kuvuka nusu ya
idadi ya wapiga kura hivyo hawakufika katika vigezo vinavyotakiwa.
Mgombea huyo anatarajiwa kwenda kuchukua fomu ya kugombea ubunge kwa
msimamizi mkuu wa uchaguzi jimbo la Handeni Mjini kesho na kuirudisha
ambapo tarehe tano wataanza kampeni rasmi.