Flatnews

HUU NDIO UPENDO WA AUNT EZEKIEL KWA MTOTO WAKE.

Mwigizaji wa filamu nchini, Aunt Ezekiel amesema mtoto wake, anamfananisha na mboni ya jicho lake. Aunt amesema amefurahi ku...


Aunt Ezekieli
Mwigizaji wa filamu nchini, Aunt Ezekiel amesema mtoto wake, anamfananisha na mboni ya jicho lake.
Aunt amesema amefurahi kujifungua salama na jukumu lililoko mbele yake ni kumlea na kumtunza mwanae ili aweze kukua katika mazingira bora.

Akizungumza kutoka jijini Dar es Salaam, Aunt alisema nguvu zake zote atazielekezea kwa mtoto wake kwasasa ili kufanya jitihada kuhakikisha mtoto wake anaishi katika mazingira mazuri.
“Nina furaha sana na mimi kuitwa mama kwani ndio ilikuwa ndoto yangu, nimeitimiza cha msingi sasa ni kumlea mwanangu katika maadili mazuri tena ya kiafrika  sijui niielezeje furaha yangu asante mungu,”alisema
Aunt alijifungua mtoto wa kike alhamisi iliyopita na amempa jina la Cookie.
Baba yake ni Moses Iyobo, mnenguaji wa Diamond.

Related

NEWS 1014212137149969170

Post a Comment

emo-but-icon

item