AMA KWELI DUNIA IKO MWISHO! MTOTO ALBINO AKUTWA AMEKATWA KICHWA NA MIGUU HUKO BIARAMURO
MTOTO YOHANA AKIWA AMEUWAWA KIKATILI KWA KUKATWA MIGUU NA MIKONO Serikali! Serikali! Serikali!
https://samchardtz.blogspot.com/2015/02/ama-kweli-dunia-iko-mwisho-mtoto-albino.html

MTOTO YOHANA AKIWA AMEUWAWA KIKATILI KWA KUKATWA MIGUU NA MIKONO
Hii Aibu ya Nchi yetu itakaisha lini Jamani?!Zamani Watu waliaminishwa
na stori kuwa Albino hafi Bali anatoweka. Ukibisha unaulizwa uonyeshe
Kaburi la Albino. Kumbe idadi yao ilikuwa chache ndio sababu ni ngumu
kufahamu.Sasa kwa matukio Haya yanayoendelea, mtafanya Watu waamini
Kwamba hili la Albino lilianza zamani kutekwa na kuuawa kikatili.
Inaumiza sana na kutia uchungu kuona ukatili na unyama wanaofanyiwa hii
jamii kwa imani za kishenzi kwenye Dunia ya Leo. Ni aibu aibu tena aibu
kubwa sana.Tunataka kuona hili jambo linakoma haraka sana. Aaaagh! Too Much sasa! Mnaudhi SANA!
ONA HII SASA......Ubinadaam ipo wapi hapa!?
Mtoto YOHANA S/0 BAHATI, 1MIAKA , albinos aliYe tekwa Chato, Geita akutwa amekatwa mikono na miguu ktk hifadhi ya Biharamulo.
Mtoto YOHANA S/0 BAHATI, 1MIAKA , albinos aliYe tekwa Chato, Geita akutwa amekatwa mikono na miguu ktk hifadhi ya Biharamulo.
Mnisamehe kwa kuweka hii Picha ya tukio, lakini imenilazim kuonyesha uchungu nilioupata dhidi ya kitendo hiki ovu.
Lazima serikali ichukue hatua haraka kukomesha ukatili huu