WASICHANA WAWILI WABAKWA NA KUUAWA.
https://samchardtz.blogspot.com/2014/05/wasichana-wawili-wabakwa-na-kuuawa.html
Watu nchini
India wameghadhabishwa na uzembe wa polisi katika jimbo la Uttar Pradesh
kufuatia tukio la wasichana wawili kubakwa na kuuawa na mili yao
kuwekwa juu ya mti.
Babayake na mmoja wa wasichana hao amesema kuwa polisi walimkejeli
alipokwenda kwao kutaka usaidizi wa kumtafuta msichana wake aliyetoweka
kabla ya kupatikana akining'inia kwenye mti na mwenzake.
Alisema kuwa wakati polisi walipogundua kuwa anatoka katika tabaka
linalotazamiwa kuwa la hadhi ya chini, walikataa kumsaidia kutafuta
msichana wake.
Watu watatu akiwemo polisi mmoja wamekamatwa kuhusiana na tukio hilo.
Familia za waathiriwa zimelalamika kwamba polisi walikataa kuwasaidia
kutafuta wasichana hao waliokuwa na umri wa miaka 14 na 16 mtawalia na
ambao pia wanatoka familia moja.
"nilipokwenda kwa polisi, kitu cha kwanza nilipoulizwa, ni tabaka
langu , nilipowaambia wakaanza kunitukana, '' alisema baba huyo wa mmoja
wa wasichana hao waliobakwa kisha kuuawa.
Polisi walisema kuwa wanaume hao walikamatwa kwa kuwabaka kisha kuwaua wasichana hao.
Polisi mmoja pia alizuiliwa kwa kushirikiana na washukiwa na pia kwa
kukosa kuchukua hatua. Bado mshukiwa mmoja anasakwa na polisi.Watu
nchini India wameghadhabishwa na uzembe wa polisi katika jimbo la Uttar
Pradesh kufuatia tukio la wasichana wawili kubakwa na kuuawa na mili yao
kuwekwa juu ya mti.
CHANZO BBC
