Flatnews

HotNews_Watatu Wakamatwa Kwa Kudurufu Kazi za Wasanii_Kigoma

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kigoma, Jaffari Mohamed, akionyesha baadhi ya CD ambazo watuhumiwa walikutwa nazo.



Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kigoma, Jaffari Mohamed, akionyesha baadhi ya CD ambazo watuhumiwa walikutwa nazo.

JESHI la Polisi Mkoani Kigoma limewakamata baadhi ya maharamia wa kazi za Wasanii ambao wanadaiwa kudurufu kazi za Wasanii na kuziuza kinyume cha Sheria.

Kamanda wa Polisi Mkoani Kigoma, Jaffari Mohamed, amesema kuwa Septemba 16 mwaka huu majira ya saa tano na nusu asubuhi katika mtaa wa Mwanga Manispaa ya Kigoma Ujiji, askari polisi waliwakamata watu watatu ambao walikuwa wakidurufu kazi za wasanii wa hapa nchini na nje ya nchi.

“Tumewakamata wakiwa na Computer Laptop 5, Desktop 4 na CD 220, wako mahabusu na tukamilisha upelelezi ili wafikishwe mahakamani,”alisema Kamanda Jaffari.

Aliwataja watu hao kuwa ni Alhamud Shabani mwenye umri wa miaka 19, mkazi wa Mlole, Abeid Adam miaka 19, mkazi wa Mwanga na Ayub Huein miaka 21, mkazi wa Mwanga Majengo Manispaa ya Kigoma Ujiji.

Post a Comment

emo-but-icon

item