Flatnews

CHUO KINGINE CHA TIBA MATATANI, CHAPIGWA MARUFUKU


Siku moja baada ya Serikali kuifungia kwa muda usiojulikana Hospitali ya Chuo cha Kimataifa cha Matibabu na Teknolojia (IMTU), kinachohusishwa na utupaji wa viungo vya binadamu mithili ya takataka, Serikali mkoani Rukwa nayo imekifungia chuo kingine cha  Rukwa College of Health and Allied Sciences.
Moja ya sababu ya kukifungia chuo hicho ni kutokuwa na kibali cha Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii huku mitaala ya kozi zake ikiwa haipo, kwa maana ya kupitwa na wakati.
Kutokana na kasoro hizo, Serikali ya mkoa kupitia Idara yake ya Afya imezuia wanafunzi wa chuo hicho kufanya mazoezi ya vitendo katika Hospitali ya Mkoa na nyingine mkoani hapa.
Chuo  hicho kinachomilikiwa  na Umoja wa Kuendeleza Wanawake Mkoani Rukwa (RWAA)  ambacho kipo  Kanondo, nje kidogo  ya Mji wa Sumbawanga, kwa sasa wanafunzi  wake wa mwaka  wa mwisho wako katika maandalizi ya mitihani yao  ya  kuhitimu  masomo. Mitihani hiyo inatarajia kuanzia Agosti 25, mwaka  huu.
Mganga Mkuu  wa Mkoa wa Rukwa, Dk John Gurisha  amelithibitishia gazeti hili juu ya uamuzi huo wa serikali ya mkoa kwa kile alichosema chuo hicho kinaendeshwa  kinyemela,  ikiwa ni  kinyume cha utaratibu  kwani hata  mitaala ya kozi  zinazofundishwa haipo katika mfumo wa masomo Tanzania,  hivyo si  rahisi kupata  viwango  vya ubora  wa  wanafunzi.
Akifafanua,  Dk Gurisha  alisema  usajili  wa muda   uliotolewa na Baraza la Mitihani la Taifa (NACTE) haukipi chuo hicho  uhalali  wa kutoa  mafunzo ya tiba,  bali  kinatoa  ruhusa ya kufungua  chuo ili kiweze kutoa  kozi  za  tiba.

Post a Comment

emo-but-icon

item