CHUO KINGINE CHA TIBA MATATANI, CHAPIGWA MARUFUKU
https://samchardtz.blogspot.com/2014/07/chuo-kingine-cha-tiba-matatani-chapigwa.html
Siku moja baada ya Serikali kuifungia kwa muda usiojulikana Hospitali ya
Chuo cha Kimataifa cha Matibabu na Teknolojia (IMTU), kinachohusishwa
na utupaji wa viungo vya binadamu mithili ya takataka, Serikali mkoani
Rukwa nayo imekifungia chuo kingine cha Rukwa College of Health and
Allied Sciences.
Moja ya sababu ya kukifungia chuo hicho ni kutokuwa na kibali cha Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii huku mitaala ya kozi zake ikiwa haipo, kwa maana ya kupitwa na wakati.
Kutokana na kasoro hizo, Serikali ya mkoa kupitia Idara yake ya Afya imezuia wanafunzi wa chuo hicho kufanya mazoezi ya vitendo katika Hospitali ya Mkoa na nyingine mkoani hapa.
Chuo hicho kinachomilikiwa na Umoja wa Kuendeleza Wanawake Mkoani Rukwa (RWAA) ambacho kipo Kanondo, nje kidogo ya Mji wa Sumbawanga, kwa sasa wanafunzi wake wa mwaka wa mwisho wako katika maandalizi ya mitihani yao ya kuhitimu masomo. Mitihani hiyo inatarajia kuanzia Agosti 25, mwaka huu.
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Dk John Gurisha amelithibitishia gazeti hili juu ya uamuzi huo wa serikali ya mkoa kwa kile alichosema chuo hicho kinaendeshwa kinyemela, ikiwa ni kinyume cha utaratibu kwani hata mitaala ya kozi zinazofundishwa haipo katika mfumo wa masomo Tanzania, hivyo si rahisi kupata viwango vya ubora wa wanafunzi.
Akifafanua, Dk Gurisha alisema usajili wa muda uliotolewa na Baraza la Mitihani la Taifa (NACTE) haukipi chuo hicho uhalali wa kutoa mafunzo ya tiba, bali kinatoa ruhusa ya kufungua chuo ili kiweze kutoa kozi za tiba.
Moja ya sababu ya kukifungia chuo hicho ni kutokuwa na kibali cha Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii huku mitaala ya kozi zake ikiwa haipo, kwa maana ya kupitwa na wakati.
Kutokana na kasoro hizo, Serikali ya mkoa kupitia Idara yake ya Afya imezuia wanafunzi wa chuo hicho kufanya mazoezi ya vitendo katika Hospitali ya Mkoa na nyingine mkoani hapa.
Chuo hicho kinachomilikiwa na Umoja wa Kuendeleza Wanawake Mkoani Rukwa (RWAA) ambacho kipo Kanondo, nje kidogo ya Mji wa Sumbawanga, kwa sasa wanafunzi wake wa mwaka wa mwisho wako katika maandalizi ya mitihani yao ya kuhitimu masomo. Mitihani hiyo inatarajia kuanzia Agosti 25, mwaka huu.
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Dk John Gurisha amelithibitishia gazeti hili juu ya uamuzi huo wa serikali ya mkoa kwa kile alichosema chuo hicho kinaendeshwa kinyemela, ikiwa ni kinyume cha utaratibu kwani hata mitaala ya kozi zinazofundishwa haipo katika mfumo wa masomo Tanzania, hivyo si rahisi kupata viwango vya ubora wa wanafunzi.
Akifafanua, Dk Gurisha alisema usajili wa muda uliotolewa na Baraza la Mitihani la Taifa (NACTE) haukipi chuo hicho uhalali wa kutoa mafunzo ya tiba, bali kinatoa ruhusa ya kufungua chuo ili kiweze kutoa kozi za tiba.