Flatnews

Sanusi achaguliwa Emir mkuu wa Kano

Sanusi sasa ndiye Kadhi mkuu wa Kano



Sanusi sasa ndiye Kadhi mkuu wa Kano

Aliyekuwa Gavana mkuu wa benki kuu ya Nigeria , Lamido Sanusi, ametajwa kuwa kadhi mpya wa Kano nchini Nigeria.
Kadhi huyo mpya aliyejiwekea taji la kuwa mhakiki mashuhuri wa serikali atakakuwa miongoni mwa viongozi wa dini wenye ushawishi mkubwa kaskazini mwa taifa hilo .
Kama gavana wa benki, Bwana Sanusi, alishutumiwa kwa madai ya ulaghai ya hali ya juu na kusimamishwa kazi mwezi Februari
Aliyekuwa kadhi hapo awali, Al-Haji Ado Bayero, aliaga dunia akiwa na miaka 83 Ijumaa baada ya kuugua kwa muda mrefu
Kwa mujibu wa mwandishi wa BBC aliyeko Abuja Tomi Oladipo, Bwana Sanusi alifanya mageuzi alipokuwa gavana wa benki ya taifa , akikabiliana na ulaghai ulioenea katika sekta ya fedha.
Sanusi sasa ndiye Kadhi mkuu wa Kano
Hivi karibuni alidai kuwa ufisadi katika sekta ya mafuta ya petrol ilimaanisha kuwa uzalishaji wa mafuta hailingani na mapato kwa hivyo mabilioni ya madola yanatoweka bila ya mtu yeyote kuwajibishwa.
Rais Goodluck Jonathan hakufurahishwa na madai hayo na hivyo kibarua chake bwana Sanusi kikaota nyasi katika benki kuu.
Kama kadhi mpya wa Kano, uhusiano kati ya Lamido Sanusi na rais Jonathan utaangaliwa kwa makini kabla ya uchaguzi wa urais mwaka ujao.
Mojawapo ya kazi ya bwana Sanusi itakuwa kusaidia kukabiliana na uasi wa kundi la wanamgambo wa Boko Haram kasazini mwa nchi hiyo.
Kundi hilo limewashutumu viongozi wa dini ya Uislamu kwa kushindwa kutekeleza tafsiri kali ya Koran.

Post a Comment

emo-but-icon

item