Flatnews

Wandili wa SEMA ajitosa kuwania ubunge jimbo la Singida mjini kwa tiketi ya ACT

Mfanyakazi wa shirika lisilo la kiserikali la SEMA mkoani Singida, Jeremiah Paul Wandili, (katikati) akitangaza nia ya kugombea u...


DSC00502

Mfanyakazi wa shirika lisilo la kiserikali la SEMA mkoani Singida, Jeremiah Paul Wandili, (katikati) akitangaza nia ya kugombea ubunge jimbo la Singida mjini kupitia tiketi ya ACT Wazalendo. Kulia ni Mwakilishi wa mwenyekiti wa ACT Wazalendo mkoa wa Singida, Peter Mkenyi na kushoto ni Mratibu wa harakati za Wandili za kugombea jimbo Peter Lisu.(Picha na Nathaniel Limu).

Na Nathaniel Limu, Singida
KIJANA mfanyakazi wa Shirika lisilo la kiserikali la SEMA Singida Mjini, Jeremiah Paul Wandili (27), amejitosa kuwania nafasi ya ubunge jimbo la Singida mjini kupitia tiketi ya ACT Wazalendo.
Wandili  amedai kuwa yeye ni kijana mwenye nguvu na afya njema na lengo lake kuu na kiu yake,ni  kuona mabadiliko makubwa kwa wananchi wa jimbo la Singida mjini.
Alizungumza na waandishi wa habari juzi, Wandili alisema amechukua uamuzi huo mzito, baada ya kujikagua na kubaini kwamba anao uwezo mzuri wa kuwatumikia wakazi wa Jimbo la Singida na  kudai  kwamba kero/ changamoto zinazowakabili wananchi, anazifahamu kwa kina.
Alisema pia amejitokeza kupitia ACT – wazalendo akiamini ndicho chama pekee chenye uwezo wa kulivusha jimbo la Singida mjini, katika matatizo mbalimbali yanayowakabili wananchi na kuleta mabadiliko makubwa mapema iwezekanavyo.
Akifafanua, Wandili alisema binafsi yeye anachukizwa na umaskini uliokithiri katika jimbo la Singida mjini, na endapo Chama chake kitampitisha na kisha wananchi wakampa ridhaa ya kuwawakilisha, vita dhidi ya umaskini, itakuwa kipaumbele chake cha kwanza.
“Nina imani kuwa wananchi wa Jimbo la Singida Mjini, wanauchukia umaskini, kwa hiyo wote wataniunga mkono katika kukabiliana na umaskini huu ambao umesababisha washindwe kuishi maisha bora”,alisema.
Alisisitiza, alisema wananchi wa Jimbo la Singida Mjini hawana budi kuachana na baadhi ya wanasiasa wanaotumia umaskini wa wananchi kama mtaji wao, katika kufanikisha malengo yao ya kisiasa.
“Nimeziona fursa mbalimbali katika jimbo letu ambazo hazijatumiwa ipasavyo, kwa imani yangu ni kwamba kama fursa hizo zitatumwa vizuri, basi zitatokomeza umaskini kwa haraka kupitia kwa wananchi wenyewe”,alisema Wandili.
Alifafanua zaidi, alisema atatumia mbinu shirikishi katika kuweka miundo mbinu rafiki itakayochangia ukuaji wa uchumi na kwa kitendo hicho, adui umaskini atatokomeza kabisa.
“Tunataka tufungue ukurasa mpya wa siasa hapa jimboni. Tutaanzisha siasa zitakazo shirikisha masuala ya vijana, wanawake, wazee, wakulima, wafanyakazi, wajasiriamali, wafanyabiashara na wote wenye mapenzi mema na maendeleo la jimbo letu, ni lengo kuu liwe ni kutokomeza umaskini”, alisema.

Related

NEWS 7052576535953321691

Post a Comment

emo-but-icon

item