ROONEY AKIJIANDAA KUICHEZEA ENGLAND MCHEZO WA 100,ATEMBELEA SHULE YAKE YA MSINGI…..
Mshambuliaji wa England Wayne Rooney akijiandaa kuandika historia ya kuwa miongoni mwa wachezaji walioichezea timu yao ya Taifa michezo 10...
http://samchardtz.blogspot.com/2014/11/rooney-akijiandaa-kuichezea-england.html

Mshambuliaji wa England Wayne Rooney akijiandaa kuandika historia ya kuwa miongoni mwa wachezaji walioichezea timu yao ya Taifa michezo 100 na zaidi.
Mara nyingi wachezaji wa England wanapokuwa wamecheza michezo 99 huwa na utamaduni wa kwenda kwenye shule zao na kupigia picha na jumla ya wanafunzi 99
England inajiandaa kucheza mchezo wa kufuzu fainali za Euro 2016 dhidi ya Slovenia mwishoni mwa juma hili kwenye dimba la Wembley,huenda Rooney ambaye pia ni nahodha wa kikosi hicho akatimiza mchezo wa 100 siku iyo na kuwa mchezaji wa 9 kuichezea England michezo 100.

Baadhi ya wachezaji wengine waliofanikiwa kuvaa jezi ya England mara 100 na zaidi katika kipindi cha miaka 142 tangu timu hiyo ianzishwe ni:

Peter Shilton, David Beckham, Steven Gerrard, Bobby Moore, Ashley Cole, Frank Lampard, Bobby Charlton na Billy Wright –
Hiyo ndio ilikuwa sababu ya Rooney kurejea kwenye shule yake ya Primary, Our Lady and St Swithin’s Catholic Primary School iliyopo kwenye jiji la Liverpool.


siku ambayo DAVID BECKHAM alikuwa nacheza mchezo wa 100 alikabidhiwa kofia ya dhahabu……..

LAMPARD pia alikabidhiwa kofia ya dhahabu kama ilivyo kawaida………..

STEVEN GERRARD pia………