MISS TANZANIA 2013 KUSHIRIKI MASHINDANO YA DUNIA DESEMBA
Miss Tanzania 2013, Happiness Watimanywa akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani).
http://samchardtz.blogspot.com/2014/11/miss-tanzania-2013-kushiriki-mashindano.html
Mwenyekiti wa kamati ya Miss Tanzania, Hashimu Lundenga, akiwa kwenye hafla hiyo.
Happiness
Watimanywa na Lundenga wakiwa meza kuu. KISURA aliyeibuka kidedea kwa
kushinda taji la Miss Tanzania mwaka 2013, Happiness Watimanywa (20),
kesho anatarajia kuondoka nchini kuelekea Uingereza katika kushiriki
mashindano ya urembo ya dunia, yatakayofanyika jijini London kuanzia
Desemba 14 mwaka huu.
Hayo yamesemwa leo na Mwenyekiti wa Kamati ya Miss Tanzania, Hashimu
Lundenga, alipokuwa akizungumza na wanahabari katika jijini Dar es
Salaam.Akizungumzia suala hilo, Happiness amesema:
“Nitajitahidi sana kuonekana katika hao warembo 130 watakaoshiriki
kwani nimejianda vizuri. Wadau na sekta mbalimbali zimeniandaa vya
kutosha wakiwemo wanamitindo wa hapa nchini kunivisha katika mashindano
hayo