Flatnews

NAY WA MITEGO KUINGIZA SOKONI MADAFTARI YAKE YA SHULE YATAITWA MR NAY

Rapper Nay wa Mitego amesema anatarajia kuzindua mradi wake wa madaftari ya shule kwaajili ya wanafunzi wa chekechea, shule ya msing...


Rapper Nay wa Mitego amesema anatarajia kuzindua mradi wake wa madaftari ya shule kwaajili ya wanafunzi wa chekechea, shule ya msingi na sekondari na vyuo vikuu.
nay-wa-mitego
Akiongea na 255 kwenye kipindi cha XXL, Clouds FM, Nay amesema pamoja na kufanya muziki yeye ni mfanyabiashara na anaamua kuwekeza ili hata kama muziki ukigoma awe ni kitu cha kumuingizia kipato.
“Nimeamua kutengeza madaftari yangu, kuna madaftari ya Mr Nay yatakuwa yanatoka. Ni madaftari ya kawaida na counter books ambazo zitakuwa zikisambazwa kuanzia nursery, primary, sekondari mpaka vyuo.
Nay amesema tayari ameshapata tenda ya kusambaza vifaa hivyo mkoani Mara. “Ni kitu ambacho tayari kiko confirmed,” amesisitiza.
Amesema madaftari hayo yataingia sokoni mwishoni mwa mwezi wa 12.

Post a Comment

emo-but-icon

item