CHADEMA KUANZA KAMPENI YA KUIKATAA KATIBA KESHO
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe akizungumza jambo katika kikao hicho kilichofanyika jijini Dar es salaam.
http://samchardtz.blogspot.com/2014/10/chadema-kuanza-kampeni-ya-kuikataa.html
Chama cha Demokrasia na maendeleo (CHADEMA) kinatarajia kuanza kesho
mchakato wa kuzunguka nchi nzima kuwaelimisha wananchi waipigie kura ya
hapana katiba iliyopendekezwa. Hatua hiyo imebainishwa kupitia kikao
cha kamati cha Chama cha Maendeleo na Demokrasia (Chadema)
iliyofikia tamati leo jijini Dares salaam.
Kwa mujibu wa Mwanasheria wa Chama hicho Tundu Lissu amesema kwamba mchakato wa kuzunguka nchi nzima kuwaelimisha wananchi waikatae katiba iliyopendekezwa umegawanyika katika makundi matatu ambayo ni kundi la Kanda ya Ziwa litakalozunguka kwa siku 20, Kundi ka Baraza la Vijana na kundi la mwisho ni kundi la Uongozi wa juu wa chama hicho.
Kuhusu suala la daftari la kupiga kura, Mbowe amesema daftari hilo linapaswa kuboreshwa kwa kuwa kuna idadi kubwa ya wananchi hawakuandikishwa, hivyo kwenye uchaguzi mkuu ujao watakosa haki yao ya kupiga kura.
Katika hatua nyingine serikali imetoa taarifa ya kuandaa utaratibu wa kupiga kura ya maoni ambapo unatarajiwa kufanyika ifikapo mwakani. Jambo lolote linaweza kutokea kwa sababu wananchi ndio waamuzi wakuu wa katiba iliyopendekezwa.
BOFYA HAPA
Kwa mujibu wa Mwanasheria wa Chama hicho Tundu Lissu amesema kwamba mchakato wa kuzunguka nchi nzima kuwaelimisha wananchi waikatae katiba iliyopendekezwa umegawanyika katika makundi matatu ambayo ni kundi la Kanda ya Ziwa litakalozunguka kwa siku 20, Kundi ka Baraza la Vijana na kundi la mwisho ni kundi la Uongozi wa juu wa chama hicho.
Kuhusu suala la daftari la kupiga kura, Mbowe amesema daftari hilo linapaswa kuboreshwa kwa kuwa kuna idadi kubwa ya wananchi hawakuandikishwa, hivyo kwenye uchaguzi mkuu ujao watakosa haki yao ya kupiga kura.
Katika hatua nyingine serikali imetoa taarifa ya kuandaa utaratibu wa kupiga kura ya maoni ambapo unatarajiwa kufanyika ifikapo mwakani. Jambo lolote linaweza kutokea kwa sababu wananchi ndio waamuzi wakuu wa katiba iliyopendekezwa.
BOFYA HAPA

