Wazee walikoroga mdahalo wa Katiba Mpya
http://samchardtz.blogspot.com/2014/08/wazee-walikoroga-mdahalo-wa-katiba-mpya.html
Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk Kitila Mkumbo
akitoa mada kwenye kongamano lililokuwa likijadili mchakato wa Katiba
Mpya, lililofanyika kwenye Ukumbi wa Nkrumah, Dar es Salaam jana. Picha
na Venance Nestory
Na Andrew Msechu na Elias Msuya
Posted Jumatatu,Agosti4 2014 saa 9:12 AM
Posted Jumatatu,Agosti4 2014 saa 9:12 AM
Kwa ufupi
Baada ya mwenyekiti wa mjadala, Profesa Francis
Mhilu kueleza kuwa ni muda wa kupata busara za wazee, alimwita mzee
George Mgodawivaha aliyesifu jitihada za Rais Jakaya Kikwete kuhakikisha
kuwa Katiba Mpya inapatikana, lakini mambo yaliharibika pale alipoanza
kumshambulia aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji
Joseph Warioba.
Dar es Salaam. Wazee walioalikwa kutoa busara
zao katika mdahalo wa Katiba jana walilikoroga baada ya kutoa maoni
ambayo yaliwakera wasikilizaji waliokuwa katika Ukumbi wa Nkrumah wa
Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), hivyo wakawazomea na kuwatimua
jukwaani.
Baada ya mwenyekiti wa mjadala, Profesa Francis
Mhilu kueleza kuwa ni muda wa kupata busara za wazee, alimwita mzee
George Mgodawivaha aliyesifu jitihada za Rais Jakaya Kikwete kuhakikisha
kuwa Katiba Mpya inapatikana, lakini mambo yaliharibika pale alipoanza
kumshambulia aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji
Joseph Warioba.
“(Rais) alimwamini sana huyu mheshimiwa Joseph
Warioba ambaye katika rasimu hii hakuitendea haki nchi,” alisema
Mgodawivaha ambaye baada ya kumaliza sentensi hiyo alizomewa na sehemu
ya wasikilizaji wakimtaka aache kupoteza muda.
Kelele zikazidi, ilibidi aondoke kwenye mimbari na
kwenda kuketi. Baada ya ‘busara’ za Mgodawihava kukataliwa, mwenyekiti
wa mdahalo alimwita, Dk Emmanuel Makaidi (Mwenyekiti wa NLD), ambaye
alianza kwa mbwembwe za kuishambulia CCM kuwa yeye hajawahi kuwa sehemu
yake tangu kabla ya uhuru.
Alisema alikuwa kwenye chama cha Congress, chini
ya Zuberi Mtemvu na kuwa tatizo lililopo ni kuwa watu wanaoharibu nchi
ndiyo leo wanaoambiwa waitengeneze.
“Hatuna Tanganyika yetu halafu mnatuambia nini,
Wasira (Stephen, Waziri Ofisi ya Rais, Uhusiano na Uratibu), sijui
anatuambia nini hapa wakati nchi ishawekwa rehani,” alisema Dk Makaidi,
kauli iliyosababisha upande mmoja wa wasikilizaji kuanza kuzomea, huku
akisisitiza kuwa anataka kumalizia hoja zake.
Hata hivyo, alikwama kuendelea baada ya kelele kuzidi na kuishia kuondolewa jukwaani kabla ya kuitwa vijana kutoa maoni yao.
Akizungumza baada ya madahalo huo, Mgodawihava
alisema Jaji Warioba alikosema kuweka kwenye Rasimu serikali tatu na
badala yake angeliwaachia wananchi wenyewe waamue kama ni mbili au tatu.
Wakati mdahalo unakaribia mwisho, wazungumzaji,
Wasira na Tundu Lissu (Chadema) wakiwa wamehitimisha mada zao, sehemu
kubwa ya wajumbe waliamua kuondoka baada ya kutolewa nafasi kwa Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi
kufunga mdahalo na alitumia nafasi hiyo kujibu hoja za Ukawa.
Baadhi ya wajumbe walimzomea lakini yeye
akawaambia waendelee kumzomea kwa kuwa alikwishazoea hali hiyo.
Akizungumza baadaye, Lukuvi aliweka bayana kuwa Bunge halitaahirishwa.
Alimnyooshea kidole Lissu kuwa ndiye “kimzizi cha
Ukawa” akifafanua kuwa kama kuna mchawi wa Ukawa, basi Lissu ndiye
mchawi namba moja, akimaanisha kuwa yeye ndiye mshawishi mkubwa wa mambo
ambayo umoja huo unayapigania.
KWA STORI KAMILI BOFYA HAPA
KWA STORI KAMILI BOFYA HAPA
