Flatnews

MAN CITY WAMTAKA SERGIO AGUERO KAUNGUKA MITANO KABLA YA KUANZA LIGI KUU ENGLAND


Hopeful: Manchester City are keen for Sergio Aguero to sign a new deal before the start of the new season
Manchester City wanamtaka Sergio Aguero asaini mkataba mpya kabla ya kuanza msimu mpya.
MANCHESTER City wanatumaini kuwa Sergio Aguero atasaini mkataba mpya utakaomfanya alipwe paundi laki mbili na elfu 10 kwa wiki kabla ya kuanza kwa msimu mpya.
Mabingwa hao wa England wameweka wazi kuwa mshambuliaji huyo wa Argentina yupo katika mipango yao ya baadaye pamoja na nahodha Vincent Kompayn na mazungumzo yanaendelea vizuri.
Barcelona na Real Madrid wameweka wazi siri ya kuvutiwa na mshambuliaji huyo mwenye miaka 26, lakini City wanafanya haraka ili kumuongezea mkataba wa miaka mitano.
Mkataba wa sasa wa Aguero unamalizika mwaka 2017, lakini Man City wanaona ni miaka michache imesalia, hivyo kuna haja ya kumuongezea tena.
Aguero alikuwa anasumbuliwa na majeruhi msimu uliopita, lakini alifunga mabao 28 katika mechi 34 alizocheza.
City wameshaanza mazungumzo ya awali na Kompany ili apewe mkataba wa miaka mitano na wanatumaini Edin Dzeko, Joe Hart na James Milner watafuatia.
Milner mwenye miaka 28, anataka kuona ni mechi ngapi atacheza kabla ya kuongeza mkataba, lakini ni mchezaji muhimu kwa City.
Waiting game: James Milner is keen to see how many games he gets before committing to Man City
Anasubiri mechi: James Milner yupo makini kuangalia ni mechi ngapi atacheza kabla ya kuongeza mkataba na kujifunga Manchester City.

Post a Comment

emo-but-icon

item