Flatnews

NZIA:- MTU MMOJA AFARIKI DUNIA PAPO HAPO KWA KUANGUKIWA NA KICHUGUU {PICHA}

Mwili wa Mkazi wa kijiji cha Ruganzo wilayani Ngara mkoani Kagera Raulian Ladislaus mwenye umri wa Miaka 40, u kiwa umeangukiwa na Ki...


Mwili wa Mkazi wa kijiji cha Ruganzo wilayani Ngara mkoani Kagera Raulian Ladislaus mwenye umri wa Miaka 40, ukiwa umeangukiwa na Kichuguu na kufariki papo hapo June 12,2014,mchana wakati akichimba kichuguu hicho kwa lengo la kuangamiza mchwa waliokuwa wakiharibu miwa yake aliyoilima  karibu kichuguu hicho.

Tukio hilo limetokea  majira ya saa 4 asubuhi wakati Marehemu akichimba kichuguu hicho ili kukihamisha kwa lengo la kusalimisha ekari moja ya Miwa iliyokuwa karibu na kichuguu hicho kabla ya kuangukiwa na kukandamizwa na Kichuguu hicho kifuani.
Baadhi ya Wananchi wa Kijiji cha Uganzo walishirikiana kuchimba kichuguu hicho kwa lengo la kumtoa marehemu ambaye alizikwa juzi June 12, 2014,Jioni Nyumbani Kwake.. ‘’Mungu ailaze mahali pema peponi.... Amina..’’

Post a Comment

emo-but-icon

item