LOWASSA ATABIRI BOMU KULIPUKA TANZANIA
Waziri Mkuu Mstaafu Mh Edward Lowassa.
http://samchardtz.blogspot.com/2014/06/lowassa-atabiri-bomu-kulipuka-tanzania.html

Waziri
Mkuu wa zamani, Edward Lowassa amesema vijana 10,500 waliojitokeza hivi
karibuni kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kufanya usaili wa nafasi
70 za kazi katika Idara ya Uhamiaji, ni ishara kuwa bomu la ajira
litalipuka muda wowote.Akizungumza
na waandishi wa habari jana nje ya Viwanja vya Bunge, Lowassa alisema
Serikali ni lazima ihakikishe inatengeneza ajira kwa kuwa kila mwaka
zaidi ya vijana 30,000 wanahitimu katika vyuo mbalimbali nchini.Wasomi
hao wa fani mbalimbali walijitokeza katika uwanja huo Ijumaa iliyopita,
kuanzia saa 12 asubuhi wakisubiri kufanyiwa usaili huo.Lowassa
ambaye alijiuzulu wadhifa wa Waziri Mkuu mwaka 2008, amenukuliwa mara
nyingi akiitaka Serikali kuchukua hatua kukabiliana na tatizo la ajira
na akisema ni bomu linalosubiri kulipuka.Mbunge
huyo wa Monduli kupitia CCM, aliwahi kuingia kwenye malumbano makali na
Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudensia Kabaka kuhusiana na suala la ajira
kwa vijana.Kabaka akiwa
bungeni, Machi 21, 2012 alitoa takwimu za namna Serikali ilivyokuwa
inatengeneza ajira kwa nia ya kumjibu Lowassa, ambaye alikuwa ameeleza
tatizo la ajira linavyowaathiri vijana.
Jana,
Lowassa kuongezeka kwa makundi ya vijana wanaopora watu katika maeneo
mbalimbali nchini ni ishara ya ukosefu wa ajira. “Watanzania sasa tupo
milioni 48 na kila mwaka vijana zaidi ya 30,000 wanahitimu vyuo vikuu na
kazi hakuna, pamoja na hilo hatuambiwi ni vijana wangapi ambao hawana
kazi,” alisema Lowassa.
Alisema
lazima Serikali itengeneze ajira kwa wananchi wake, huku akimtolea mfano
Rais wa Marekani, Barack Obama kwamba alishinda awamu ya pili kwa
sababu ya kutengeneza ajira.
“Mfano
mzuri ni katika uanzishwaji wa viwanda. Tunapofikiria kuanzisha kiwanda
cha pamba kwanza lazima tuangalie tutatengeneza ajira ngapi,” alisema.
Katika
kuonyesha kuwa ajira sasa ni tatizo nchini, juzi jioni wakati wa mjadala
wa Bajeti Kuu, Naibu Spika Job Ndugai alisema Mtanzania mwenye nia ya
kugombea urais mwaka 2015 ili aweze kuelekewa kwa wananchi ni lazima
aeleze mikakati ya kuwasaidia vijana kupata ajira.
“Ajira ni
tatizo kubwa na lazima lishughulikiwe. Kuna vijana hawaendi shule
lazima watazamwe. Kuna wanaomaliza darasa la saba, kidato cha nne, cha
sita na vyuo vikuu. Nazungumza kutoka moyoni kabisa. Hizi ni dakika za
mwisho za Serikali ya awamu ya nne, wale wanaojipanga kwa awamu ya tano
kama hawataongelea ajira basi waandike wameumia.”
Ndugai
alisema vijana wasio na kazi ndiyo wapigakura wakubwa na kusisitiza kuwa
mgombea yeyote makini ni lazima afikirie suala la ajira kwa vijana.