Flatnews

KUTOKA BRAZIL 2014: Ronaldo analisha walala nje wa mitaani


 
  • Staa wa zamani wa Brazil, Ronaldo de Lima anashirikiana na Serikali ya Brazil katika mpango maalumu wa kuwalisha watu wote wanaolala nje katika mitaa ya Brazil kutokana na umaskini uliosababisha ukosefu wa makazi.
hareKWELI unaouna lakini Mtanzania mmoja anayeishi vyema hapa jijini Sao Paulo ameniambia kuwa watu wanaolala nje katika miji ya Brazil wanakula vizuri kuliko baadhi ya Watanzania waliozamia hapa kutafuta maisha.
Staa wa zamani wa Brazil, Ronaldo de Lima anashirikiana na Serikali ya Brazil katika mpango maalumu wa kuwalisha watu wote wanaolala nje katika mitaa ya Brazil kutokana na umaskini uliosababisha ukosefu wa makazi.
“Hao jamaa wanaolala nje usiwaone hivyo, wanakula vizuri kuliko baadhi ya Watanzania waliokuja kutafuta maisha hapa. Kuna gari maalumu linapitia kuwaletea Wali, Nyama, Chips, Matunda, Kuku na kila aina ya chakula kizuri.” Ananiambia Mtanzania huyo wakati tukikata mitaa huku akiomba nisimtaje jina.
“Wamewekewa hoteli yao ambayo wanaweza kwenda kula bure, lakini wenyewe tu wamekuwa wavivu. Wakilala hawataki kuamka kwenda kula na ndiyo maana badala yake huwa wanaletewa vyakula.”
“Kuna hoteli nyingine wanaweza kwenda kula chakula na kulipa Rias moja tu kwa sahani. Ronaldo ndiye anashirikiana na Serikali katika mpango huo maalumu na kuna siku nyingine yeye mwenyewe huwa anatembea mitaani kugawa chakula hicho.” Jioni ya siku hii hii ninayopata habari hii ndio napata bahati ya kuona wimbo mmoja wa kundi la wanamuziki wa Brazil huku staa mwingine wa zamani wa Brazil, Ronaldinho akiimba. Naambiwa kuwa ndio kazi yake kubwa siku hizi. Mambo ya mpira amepunguza kwa kiasi kikubwa na badala yake mbwembwe zake amezidisha nje ya uwanja.
Ronaldo anaonekana kuwa bize na masuala ya Jamii, lakini inadaiwa kuwa Ronaldinho yuko bize kweli kweli na masuala ya starehe na ndiyo maana licha ya urafiki wa muda mrefu na kocha Fillipe Scolari, lakini alimwambia mapema kuwa hatamchukua katika fainali za kombe la dunia.
Anachofanya Ronaldinho ni kuongeza mauzo ya wanamuziki wa Brazil kwa kuimba vipande vya nyimbo zao huku akionekana katika video na nyimbo nzima inapata mvuto. Kazi hiyo pia anaifanya staa mwingine wa zamani wa Brazil, Adriano.
Kitu kinachovutia kutoka kwa mastaa wa Brazil ni ukweli kwamba wanapomaliza maisha yao ya soka Ulaya na kwingineko wote huwa wanarudi zao nyumbani kula raha. Ni tofauti na mastaa wa Afrika ambao wengine wanaamua kubaki Ulaya, hasa wale ambao mataifa yao yalitawaliwa na Wafaransa.

Post a Comment

emo-but-icon

item