http://samchardtz.blogspot.com/2014/06/hofu-yatanda-ya-kitu-kinachohisiwa-bomu.html
HUKU
watu karibia 60 nchini kenya wakiuawa kwenye mashambulizi ya kigaidi,
katika hali isiyo ya kawaida nchini Tanzania, walinzi wa Maduka ya
Mlimani City jijini Dar wamejikuta wakipata mchecheto wa aina yake baada
ya kitu kilichodhaniwa ni bomu kukutwa kwenye eneo la kuegeshea
magari.
Walinzi wa maduka ya Mlimani City jijini Dar wakikagua kitu kinachosadikika kuwa ni bomu.Tukio
hilo lilitokea Juni 16, mwaka huu ambapo kwa mujibu wa shuhuda
aliyeomba kusitiriwa jina, aliona gari dogo jeupe likiangusha kifaa
hicho kilichodhaniwa ni bomu kisha likatoweka.