Flatnews

FIRKA NJE YA BOKSI: BADILI CHANZO CHA TAARIFA (7)

Baada ya kutazama fikra tata na chanzo sahihi na kisicho sahihi wiki iliyopita ( bofya hapa kusoma ), leo tunaendelea na vyanzo vya mu...


Baada ya kutazama fikra tata na chanzo sahihi na kisicho sahihi wiki iliyopita (bofya hapa kusoma), leo tunaendelea na vyanzo vya muono wako juu yako.
 
VYANZO VYA MUONO WAKO JUU YAKO

1. MAWAZO/FIKRA MGANDO: 
Fikra mgando hii si kwa watu wasiowaza sahihi tu,inawezekana na wewe unawaza kwa namna iliyosahihi lakini fikara yako ni mgando.Fikra mgando ni ile hali ya mtu kuridhika na kile kitu alichonacho hata kama ni sahihi.Aina ya ulimwengu tunaoishi hata ulimwengu uliopita siku hazigandi na wala hazitakoma kama jinsi vile sekunde zinavyotembea na kuzaa dakika dakika nazo kwa muendelezo wake hivyo ndivyo fikra yako inavyotakiwa kufanya kazi na kuchakata mambo.Kama jinsi vile ulimwengu unavyobadilika ndivyo hivyo na taarifa hubadilika inaweza ikawa ni kweli kwamba jna ulifanya jambo kwa njia hiyo na likawa ni sahihi lakini kuna uwezekano mkubwa jambo lile lile ukajaribu kulifanya kwa njia ile ulioitumia jan na lisilete matokeo sahihi uliyoyategemea,Hii inatufunza hapa kwamba tunatakiwa kujiongeza katika fikra zetu tuiruhusu fikra kuwaza tene ne tena na kuruhusu kupokea fikra sahihi na mpya kila siku ili tuondokane na fikra mgando. kuna baadhi ya watu wakikosea jambo na ukitaka kuwasahihisha jibu lao hua ‘MIMI/SISI NDO WA HIVI HIVI AU HIVI NDIVYO HUA TUNAFANYA’.Unaona aina hii ya kauli inajumuisha kundi flani la watu ambao wao wanaamini kwamba ndio wa hivyo hivyo.Ukiamini kwamba wewe ndo wa hivyo hivyo ulivyo basi maisha yako na muono wao juu yako utakua hivyo hivyo jinsi ulivyo na hata kama ni kweli unawaza sawa lakini kwasababu hujaruhusu taarifa mpya iliosahihi kukufikia utaendelea kuwaza mawazo sahihi lakini mawazo mgando au mawazo yaliopitwa na wakati.


2. KUIDANGANYA NAFSI YAKO: 
Inaweza ikawa ni kauli ngumu na ngeni pia kwamba ni kwa namna gani mtu anaweza kuidanganya nafsi yake,Nataka nikujuze tu kwamba ni mara nyingi sana tumekua tukifanya hivyo bila hat kujua wakati mwingine.Kuna namna ambayo unajihisi upungufu wa kitu fulani ndani ya nafsi yako au unasikia kabisa ndani yako kuna jambo linakataa laqkini kwasababu fulani binafsi unatoa matokeo tofauti kwa nje.Mfano rahisi ni huu....unaweza ukahisi kabisa ndani ya nafsi yako kwamba sijisikii upendo wa kimahusiano na mtu fulani anaweza kua ni mwanamke au mwanaume lakini kwasababu pengine za uwezo wa kifedha au nafasi alionayo au kuna vitu unavihitaji kutoka kwake unajikuta unalazimisha hali ya kujihisi unapenda wakati ukweki wa ndani ya nafsi unakataa huku ndiko kuidanganya nafsi yako.Au wakati mwingine mtu unaweza ukawa unajijua una tatizo fulani na kulingana na lile tatizo ulilonalo kuna aina fulani ya maisha unatakiwa kuishi,lakini unakua na ki hali fulani cha kutojali au kupotezea uhalisia wa ndani na kuyafuata matakwa yako ya nje.Kuna baadhi ya watu mnaweza kujiuliza lakini hii unayoisema si ni IMANI?Jibu ni rahisi sana kwamba HAPANA hii si imani kwasababu imani haipingi ukweli uliopo lakini imani inaanza kufanya kazi pale ukweli wa japo unapoishia,kwamba ni kweli kwamba ninaumwa na kwa ugonjwa huu madaktari wanasema siwezi kupona na ndivyo ilivyo sasa imani hapa inaanzia hapa...Ni kweli madaktari wamenipima na hali yangu si nzuri lakini.... kutokana na......Ninaamini kwamba nitapona..Kwasababu ya..!Imani mara zote ni lazima iwe na viambatanishi na imani haipingani na ukweli lakini imani inasema kinyume na hali halisi na kufanya yasiyowezekana kuwezekana. 
JINSI YA KUBADILI MUONO WAKO WA NDANI

1. TAFUTA TAARIFA MPYA
Moja kati ya vitu vinatukwamisha sana katika maisha yetu pale inapofikia mahali ntu unadhani umejitosheleza kwa kila kitu hasa kwenye sehemu ya taarifa za maarifa.Kama jinsi ambavyo nilisema mwanzo kwamba ulimwengu haujaganda hivyo pia ubongo wako hautakiwi kuganda kwa taarifa ile ile ilioisikia jana na kutaka ikuletee matokeo mapya, ukitaka matokeo mapya tafuta taarifa mpya.Hivi ndivyo watu waliofanikiwa kwenye maeneno mbali mbali wanavyoishi hakuna wakati ulifika wakakaa chini na kuridhika,kuridhika ni tabia ya umasikini tafuta maarifa mapya kila siku tafuta changamoto mpya hiyo itakusaidia sana kubadili muono wako juu yako
Tukutane wiki ijayo ambapo tutaendelea kutazama namna ya kubadili muono wako wa ndani..
Unaweza kuwasiliana na mwandishi kupitia namba 0653-318117, ama kwa barua pepe fredymsungu@gmail.com 

Post a Comment

emo-but-icon

item