BAADA YA POLISI KUYAFANYIA "UMAFIA" MALORI YALIYOKUWA YAKIEGESHWA BARABARANI SASA YATII SHERIA, JIONEE MWENYEWE
http://samchardtz.blogspot.com/2014/06/baada-ya-polisi-kuyafanyia-umafia.html
Barabara nyeupeeeeeeee
Kufuatia
askari wa usalama barabarani jijini Dar es Salaam kuamua kuyafanyia
"umafia" malori yanayoegeshwa barabarani eneo la tabata relini, kwa
kufungua namba na kuondoka nazo, hivi sasa madereva hao wameshika adabu
na kufuata sheria inavyosema
Mwandishi
wa eddy blog aliyepita eneo hilo hii leo ameshuhudia malori hayo yakiwa
yameegeshwa nje ya barabara na kupelekea magari yanayotumia barabara
hiyo ya mandela kupita kwa raha tofauti na awali
Kutokana
na askari kuwapa onyo na faini za mara kwa mara pasipo mabadiliko
yeyote walilazimika kuzifungua namba za usajili za malori hayo na
kuondoka nazo, jambo lililoonekana kuwa mwarobaini wa wao kutii sheria
bila shuruti na kuegesha malori yao nje ya hifadhi ya barabara kama
picha hizo hapo juu zinavyoonesha
Mwanzoni
malori hayo yalikuwa yakiegeshwa barabarani kwa muda mrefu yakisubiri
kwenda kupakia mizigo hali iliyokuwa ikisababisha ajali za mara kwa mara
pamoja na usumbufu uzio wa lazima wa matumizi ya barabara hiyo



