WAJASIRIAMALI WALEMAVU WAFUNGA BARABARA DAR
http://samchardtz.blogspot.com/2014/05/wajasiriamali-walemavu-wafunga-barabara.html
KUNDI la
walemavu, wajasiriamali na wafanyabiashara ndogo ndogo jana walifunga
makutano ya barabara ya Kawawa na Uhuru (Karume) kwa muda wa saa tatu
wakishinikiza Serikali iwapatie maeneo ya kufanyia biashara baada ya
kuwaondoa katika eneo la Mtaa wa Kongo Kariakoo jijini Dar es Salaam.