HATIMAYE WILAYA YA KILOLO YAMILIKISHA MTO KWA MWEKEZAJI
http://samchardtz.blogspot.com/2014/05/hatimaye-wilaya-ya-kilolo-yamilikisha.html
Shamba la vitunguu

Msimamizi
wa shamba la vitunguu la mwekezaji, Onesmo Kihaga ambaye pia ni
mtaalamu wa kilimo cha umwagiliaji kisichotumia mashine akionyesha bomba
linalosafisha maji kutoka bwawani kwenda shambani.

Chanzo cha maji kabla yakuchepushwa.

Bwawa la maji
Na Matias Kanali
Wananchi
wa Kijiji cha Kitelewasi Kata ya Ilole wilayani KILOLO mkoani Iringa
wameulalamikia uongozi wa kijiji hicho kwa kubinafsisha mto wa maji na
kusababisha umasikini kwa wananchi wa kijiji hicho. (FS)


Wakala wa kiungo wa Machester City Yaya Toure amekashifu kupuuzwa kwa kiungo huyo kutoka Ivory Coast.
Dimitri Seluk alikashifu ujumbe wa
kheri njema kwa Toure ambaye alikuwa anaadhimisha siku kuu ya kutimiza
miaka 31 mnamo mei tarehe 13.Ujumbe huo ulioambatana na keki haukumridhisha hata kidogo Seluk ambaye anasema kuwa alitarajia wamiliki wa klabu hicho angalau kumtambua kiungo huyo wa Ivory Coast ,timu hiyo ilipotua Abu Dhabi kusheherekea ushindi wao wa taji la Uingereza kwa mara ya pili katika kipindi cha miaka mitatu.
Seluk alisema Toure huenda akaondoka iwapo wamiliki wa klabu hiyo wataendelea kumpuuza.
Toure aliandikisha kandarasi mpya ya miaka minne mwaka uliopita licha ya Seluk ambaye amemuakilisha Toure kwa zaidi ya miaka kumi kutishia kuwa kiungo huyo wa Ivory Coast angehama Etihad.
Uhusiano baina ya mchezaji huyo bora barani Afrika na Seluk umedumu kwa miaka mingi kiasi ya kuwa Toure alimpa mwanawe wa pili jina la Seluk.CHANZO BBC,(A.I)

Watu 17 wameuawa katika shambulizi lililofanywa dhidi ya kijiji kimoja Kaskazini Mashariki mwa Nigeria.
Mji wa Alagarno ambao uko katika jimbo
la Borno, uko karibu na mji wa Chibok ambako wasichana zaidi ya
miambili walitekwa nyara na kundi la wapiganaji wa kiisilamu la Boko
Haram wiki tano zilizopita.Hili ni shambulizi la hivi karibuni kufanywa nchini Nigeria wakati nchi hiyo ikikumbwa na kitendawili cha kuwatafuta zaidi ya wasichana miambili waliotekwa nyara na Boko Haram.
Juhudi hizo zinawashikirisha wataalamu wa ujasusi wa kimataifa kutoka Israel, Marekani na Uingereza.
Pia limetokea siku moja tu baada ya milipuko miwili kutokea mjini Jos katika jimbo la Plateau ambapo takriban watu 118 waliuawa Jumanne usiku.
Juhudi za kuwatafuta maiti bado zinaendelea.
Mwandishi wa BBC nchini Nigeria anasema kuwa shambulizi lililofanyika mjini Jos, lilisababishwa na Boko Haram na kwamba huenda ni ujumbe kwa serikali kuwa wapiganaji hao wanaweza kushambulia wakati wowote wanapotaka.CHANZO BBC,(A.I)

Mbu hawa wananofiwa kuanza kusababisha Malaria

Viini vinavyosababisha Malaria
Utafiti uliofanywa nchini Uingereza unaonyesha kuwa Mbu wameanza kuvamia maeneo mbali mbali ya nchi hiyo.
Mabadiliko katika hewa ya mjini nchini
Uingereza yameanza kutoa mazingira mazuri kwa Mbbu kuishi, ikiwemo wale
wenye uwezo wa kuambukiza ugonjwa wa Malaria na virusi vijulikanavyo
kama 'West Nile virus'.Utafiti unasema kuwa mazingira ya joto pamoja na vidimbwi vya maji katika nyumba za watu, yanawaleta Mbu karibu na watu.
Mbu wanaopatikana nchini Uingereza hawana uwezo wa kuambukiza maradhi yoyote, lakini wanasayansi hao wanasema kuwa jambo la wadudu hao kuzaana katika maeneo ya mjini linaongeza uwezo wa magonjwa kulipuka.
Wanasayansi hao hata hivyo wanakusanya data zaidi kuona ikiwa wengi wa wadudu pamoja na aina ya wadudu wenyewe inaweza kuchangia kwa vyovyote mlipuko wa maradhi au la, hasa katika maeneo ya mjini.
Kadhalika wanasayansi hao wanasema kuwa kutokana na ongezeko la viwango vya joto katika maeneo ya mjini,Mbu katika baadhi ya maeneo kama vile Kusini mwa Ulaya wameweza kusababisha magonjwa.
Pia wanasisitiza kwamba Magonjwa yamelipuka katika baadhi ya mataifa ya Ulaya kutokana na mabadiliko ya tabia ya Mbu.
Zaidi ya aina 30 ya Mmbu wamepatikana nchini Uingereza
"katika maeneo ya vijijini kuna Mmbu wengi zaidi kwa sababu ya mazingira tofauti tofauti, wengine wanapenda kuishi katika nyasi , wengine katika vidimbwi, na wengine katika mashimo,'' alisema mmoja wa wataalamu.
"lakini ukienda katika maeneo ya mijini , hakuna Mmbu wengi sana , labda utapa aina mbili au tatu ya Mmbu.
Daktari mmoja kwa jina Callaghan, alisema kuwa kulikuwa na visa vingi vya ugonjwa wa Malaria kila mwaka nchini Uingereza , wengi wanaokuwa wanarejea kutoka sehemu mbali mbali za dunia ambako ugonjwa Malaria unapatikana.CHANZO BBC,(A.I)

Dola bilioni nne za kimarekani kwa miundo msingi Ethiopia

Ethiopia inajitahidi kuimarisha miundo mbinu

Changamoto hazikosekani katika kukuwa kwa uchumi huo
Miaka
thelathini baada ya Ethiopia kukabiliwa na njaa iliyowauwa raia wengi,
nchi hio ambayo ilitambulika kwa umaskini wa kukithiri sasa imeimarika
na kuwa moja wapo ya nchi yenye uchumi unaokuwa kwa kasi zaidi barani
Afrika.
Ethiopia sasa imeanzisha mradi wa maendeleo wa kuboresha miundo mbinu ili kuinua maisha ya watu millioni 90 wa nchi hiyo.
Uchumi wa Ethiopia umeimarika katika
kipindi cha miaka saba iliyopita huku shirika la fedha duniani, IMF
likisema viwango vya ukuaji vimeongezeka kwa asilimia saba kila mwaka.Na ni katika sekta ya ujenzi ambapo ukuaji huo umeshuhudiwa zaidi.
Maendeleo nchini
Ujenzi wa majumba makubwa, maeneo ya burudani na nyumba za wapangaji umeongezeka pakubwa.
Aidha ujenzi wa miundo msingi pia umetiliwa maanani.
Mwaka huu pekee, serikali ya Ethiopia imetenga takriban dola bilioni nne za kimarekani kwa ajili ya ujenzi huo.
Waziri wa fedha nchini humo, Sufian Ahmed anasema serikali itaendelea kuwekeza katika barabara na reli.
Tayari ujenzi wa reli katika mji mkuu wa Addis Ababa, umeanza na unatarajiwa kukamilishwa mwaka ujao.
Mradi huo utagharimu takribani dola milioni mia tano.
Changamoto
Licha ya hatua hizo, viwango vya umaskini ni vikubwa Ethiopia na serikali imeendelea kukabiliwa na changamoto kubwa katika kupambana na mfumuko wa bei za bidha muhimu.
Ni suala ambalo waziri Ahmed anasema serikali inalitilia maanani.
Licha ya Ethiopia kukabiliwa na changamoto hizo, inasema imo katika mkondo wa kuwa taifa lenye utajiri wa kadri kufikia mwaka wa 2025.BBC,(A.I)

Hosni Mubarak wakati kesi yake ilipokuwa inaendelea
Rais aliyeondolewa madarakani nchini Misri, Hosni Mubarak amehukumiwa jela miaka mitatu.
Wanawe wawili Alaa na Gamal wamepata kifungo cha miaka minne kila mmoja.Wendesha mashitaka walisema kuwa wanawe Mubarak waliponda mamilioni ya dola pesa za umma zilizotengewa kukarabati ikulu ya Rais na badala yake wakafanyia ukarabati nyumba zao za kifahari.
Wametakiwa kulipa pesa hizo za serikali na kutozwa faini ya dola milioni tatu.CHANZO BBC,(A.I)

Bunge
lilipitisha makadirio ya mapato na matumizi ya wizara hiyo kwa mwaka wa
fedha 2014/15 ya Sh bilioni 799 zikiwamo Sh bilioni 344.2 za matumizi ya
kawaida na Sh bilioni 454.8 kwa ajili ya maendeleo.(Martha Magessa)
WIZARA ya Viwanda na Biashara imewasilisha bungeni bajeti yake inayoonesha mapinduzi makubwa katika viwanda, ikiwamo kuanza kwa miradi ya chuma ya Liganga na Mchuchuma na kiwanda cha kuua viluwiluwi vya mbu waenezao malaria.
Pia
kiwanda cha matairi cha General Tyre kinatarajiwa kuanza tena uzalishaji
katika mwaka ujao wa fedha. Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk Abdallah
Kigoda aliwasilisha bajeti yake hiyo bungeni jana.(Martha Magessa)

USHIRIKA
wa wachungaji wa Kipentekoste nchini (PPFT) umemtaka Kiongozi Mkuu wa
Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship (FGBF), Askofu Zakaria Kakobe,
kuacha tabia ya kutumia mwavuli wa dini kuhubiri chuki na uchochezi kwa
wananchi.
Akizungumza
juzi wakati wa kufunga semina ya viongozi wa dini wa Mkoa wa
Kilimanjaro iliyofanyika katika ukumbi wa Umoja Hostel, Mwenyekiti wa
Ushirika wa Wachungaji nchini, Askofu Ikongo alisema kauli za Askofu
Kakobe zimekuwa za hatari na zinaweza kuliingiza Taifa kwenye machafuko
ya kidini.
"Nchi
yetu imekuwa na dalili za viashiria vya kutoweka kwa amani na utulivu,
kutokana na baadhi ya viongozi wa dini kujiingiza kwenye siasa na kuanza
kutoa kauli za kuashiria uchochezi na kupandikiza chuki kwa
waumini…sasa umefika wakati sisi viongozi wa dini hatuwezi kunyamaza
kwani tutaonekana na matamko yanayotolewa kiholela kwa kutumia mwamvuli
wa upentekoste," alisema Askofu Ikongo.
Alisema
Askofu Kakobe amekiuka uadilifu wake, kwani Aprili 20 mwaka huu katika
kanisa lake la Mwenge, alitoa kauli kuwa atapambana hadi Tanganyika
irudi hata kwa kukatwa kichwa, kauli ambayo inadhihirisha ugaidi.
Askofu
Ikongo alisema kauli kama hiyo haistahili kutolewa na mtumishi yeyote wa
Mungu, kwani mtu mwenye uwezo wa kusema hata akatwe kichwa sio wa
kawaida bali ni mtu aliye na mafunzo ya kujitoa mhanga kama gaidi.
"Tunasikitishwa
na kauli za Askofu Kakobe ambazo zinaweza kuliletea Taifa machafuko ya
kidini…siku ya Pasaka Aprili 20 mwaka huu aligeuza mimbari kuwa jukwaa
la siasa, kwa kuhubiri uchochezi kwa kudai; kila mtu anayepigania kurudi
kwa Tanganyika, ana Mungu ndani yake,” alisema.
Kwa
mujibu wa Askofu Ikongo, kauli hizo za Kakobe ni za kigaidi na zina nia
ya kuvuruga amani ya Watanzania na kuliingiza taifa kwenye machafuko,
ambayo yataharibu tunu iliyoachwa na Baba wa Taifa Mwalimu Julius
Nyerere.
Alisema
ni vyema viongozi wa dini wajikumbushe wajibu wao wa kuliombea Taifa, na
kuwaongoza waumini wao kufuata yaliyo mema badala ya kugeuka sehemu ya
kutumiwa na wanasiasa.(Martha Magessa)

Dar es Salaam. Mabalozi 12 wa Umoja wa Ulaya (EU), nchini wamemtumia Waziri Mkuu, Mizengo Pinda barua ya wazi wakimtaka kuchukua hatua stahiki kwa watu waliofanya mauaji ya albino wilayani Bariadi, mkoani Simiyu.
“Tumesikitishwa na mauaji ya kikatili ya albino Munghu Lugata yaliyotokea Mei 12, 2014 wilayani Bariadi,” ilieleza sehemu ya barua hiyo iliyosainiwa na mabalozi 12 wa nchi wanachama wa EU Tanzania, wakiongozwa na Balozi wa Umoja huo nchini, Filiberto Sebregondi. (J M)

Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Lazaro Nyalandu akimsikiliza kwa makini Meneja Mkuu wa KLM kwa upande wa Africa Mashariki Bw. Dries Klein wakati hafla ya maadhimisho ya kutimiza miaka 45 ya Shirika la KLM kufanya kazi nchini yaliyofanyika jana jijijni Dar es Salaam.

Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Lazaro Nyalandu akipongezana kwa furaha na baadhi ya Wadau na watendaji wa Shirika la Ndege KLM wakati wa hafla ya maadhimisho maadhimisho ya kutimiza miaka 45 ya Shirika la KLM kufanya kazi nchini yaliyofanyika jana jijijni Dar es Salaam.

Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe Lazaro Nyalandu akipokea zawadi ya mfano wa picha ya Ndege ya Shirika la KLM katika kilele cha madhimisho ya miaka 45 ya Shirika la KLM kufanya kazi nchini yaliyofanyika jana jijijni Dar es Salaam (J M)
Canzo Fullshangwe

Waziri wa Chakula na Ushirika, Mhandisi Christopher Chiza.PICHA|MAKTABA
Dar es Salaam. Ongezeko la idadi ya
Vyama vya Ushirika wa Akiba na Mikopo (Saccos), limedaiwa kutokuwa na
msaada mkubwa kwa wajasiriamali wadogo.Kauli hiyo imekuja huku serikali kupitia Waziri wa Chakula na Ushirika, Mhandisi Christopher Chiza ikisema vyama hivyo vimeongezeka kutoka 5,424 Machi 2012 hadi 5,559 Machi 2013. (J M)


Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadiki akiungana na Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Yusuph Mwenda walipoungana na wananchi kufanya usafi katika mto wa Mlalakuwa jijini Dar es Salaam ili kuepukana na ugonjwa uliozuka wa Dengue ambao umekuwa tishio wakati akizindua zoezi la kufanya usafi jijini lililokwenda kwa jina la ‘MLALAKUWA MTO WETU, AFYA YETU’ lililofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita.

Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Yusuph Mwenda (kushoto) akimuongoza Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadiki (katikati) kukagua mto wa Mlalakuwa jijini Dar es Salaam wakati akizindua zoezi la kufanya usafi lililokwenda kwa jina la ‘MLALAKUWA MTO WETU, AFYA YETU’ lililofanyika lililofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita.
Chanzo full shwangwe. (J M)

Arusha. Maelfu ya watu wamemiminika tena katika eneo la Samunge, Wilaya ya Ngorongoro Mkoa wa Arusha, safari hii siyo kunywa Kikombe cha Babu Mchungaji Ambilikile Mwasapile, bali kupata dhahabu inayodaiwa kugundulika katika eneo hilo. (J M)

Mwanza. Siku kama ya leo mwaka 1996, ilikuwa ni vilio kila kona ya nchi, lakini Kanda ya Ziwa iliathirika zaidi na kuzama kwa meli ya Mv Bukoba na kuteketeza mamia ya wananchi. (J M)
More...
Tafuta Habari

Nafasi za Kazi & Masomo
Prev
Next
Video Gallery
Kwa video za matukio mbalimbali yanoyotokea Tanzania.

