SERIKALI YA TANZANIA YAITUNUKU HUAWEI TUZO YA UONGOZI BORA NA MCHANGO MKUBWA KATIKA SEKTA YA TEKNOLOJIA NA MAWASILIANO
Mkuu wa masuala ya ufumbuzi na ushauri wa Huawei Afrika mashariki na kusini Dr. Bello Moussa, akizungumza wakati wa mkutano wa sik...
https://samchardtz.blogspot.com/2015/08/serikali-ya-tanzania-yaitunuku-huawei.html
Mkuu
wa masuala ya ufumbuzi na ushauri wa Huawei Afrika mashariki na kusini
Dr. Bello Moussa, akizungumza wakati wa mkutano wa siku mbili wa
kimataifa ulipewa jina la Connect to Connect (C2C) ulioandaliwa na
Wizara ya Mawasiliano na teknolojia kujadili changamoto za mawasiliano
pamoja na ukuaji wa broadband katika nchi za Afrika. Mkutano ulifanyika
katika hoteli ya kimataifa ya Ramada Resort jijini Dar es Salaam.
Meneja
Uhusiano Huawei Tanzania Bw. Jimmy Nlinguo akipokea tuzo ya uongozi
bora kutoka kwa Kaimu Katibu Mkuu, Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na
Teknolojia, Selina M. Lyimo kutokana na mchango mkubwa wa kampuni hiyo
katika sekta ya teknolojia na mawasiliano hapa nchini. Tuzo hiyo
ilitolewa wakati wa mkutano wa siku mbili wa kimataifa wa Connect to
Connect (C2C) ulioandaliwa na wizara hiyo katika hoteli ya kimataifa ya
Ramada Resort jijini Dar es Salaam kujadili changamoto za mawasiliano
pamoja na jinsi ya kuongeza ukuaji wa broadband katika nchi za Afrika.
Meneja
Uhusiano wa Huawei Tanzania akisema maneno machache ya shukrani kwa
wadau wa sekta ya mawasiliano na teknolojia mara baada ya kampuni yake
kutunikiwa tuzo ya uongozi bora na Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na
Teknolojia kutokana na mchango mkubwa wa kampuni hiyo katika sekta ya
teknolojia na mawasiliano hapa nchini. Tuzo hiyo ilitolewa wakati wa
mkutano wa siku mbili wa kimataifa wa Connect to Connect (C2C)
ulioandaliwa na wizara hiyo katika hoteli ya kimataifa ya Ramada Resort
jijini Dar es Salaam.
Mkuu
wa masuala ya ufumbuzi na ushauri wa Huawei Afrika Mashariki na kusini
Dr. Bello Moussa, akijibu maswali ya waandishi wa habari muda mfupi
baada ya kutoa hotuba yake kwenye mkutano wa kimataifa uliondaliwa na
wizara ya mawasiliano, sayansi na teknolojia uliopewa jina la “Connect
to Connect (C2C)” uliofanyika katika hoteli ya kimataifa ya Ramada
Resort jijini Dar es Salaam.
Meneja
Uhusiano wa Huawei Tanzania akiongea na waandishi wa habari mara baada
ya kampuni yake kutunikiwa tuzo ya uongozi bora na Wizara ya
Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia kutokana na mchango mkubwa wa kampuni
hiyo katika sekta ya teknolojia na mawasiliano hapa nchini. Tuzo hiyo
ilitolewa wakati wa mkutano wa kimataifa wa Connect to Connect (C2C)
uliofanyika katika hoteli ya Ramada jijini Dar es salaam.
Kampuni
inayongoza katika sekta ya teknolojia na mawasiliano nchini Tanzania
(Huawei) imetunikiwa tuzo ya uongozi bora kutokana na mchango wao mkubwa
sekta ya teknolojia na mawasiliano hapa nchini.
Tuzo
hiyo imetolewa siku ya jana katika hoteli ya kimataifa ya Ramada jijini
Dar es salaam ambapo mkutano wa kimataifa wa siku mbili unaendelea.
Wizara ya mawasiliano na teknolojia huadhimisha mkutano huo kila mwaka
kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa sekta hiyo.
Mkutano
huo umewaleta pamoja wadau katika sekta ya teknolojia na mawasiliano,
watunga sera, wawekezaji pamoja na wafumbuzi mbalimbali kwa nia ya
kujadili mbinu za kukuza teknolojia ya ‘Broadband’ kati ya nchi na nchi
barani Afrika, kutoka pwani hadi pwani na uvumbuzi utakaosaidia kusukuma
uchumi wa Tanzania na kukuza ubora wa huduma za jamii.
Huawei
walipokea tuzo hiyo kutoka Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia
baada ya kuwa mstari wa mbele katika sekta ya teknolojia sayansi na
mawasiliano pamoja na kuwa kiongozi katika utafiti na kuchangia katika
ukuaji na usambazaji wa teknolojia ya broadband nchini Tanzania.
Akizungumza
wakati wa mkutano huo, Mkuu wa masuala ya ufumbuzi na ushauri wa Huawei
Afrika Mashariki na Kusini, Dr. Bello Moussa alisema “ Nchi za
Mashariki na Kusini mwa Afrika katika miaka ya hivi karibuni zimeonyesha
shauku kubwa kwenye kuwekeza na kukuza teknolojia ya broadband.
Changamoto ni kwamba nchi hizi zipo katika hatua tofauti ya maendeleo ya
teknolojia ya taarifa na mawasiliano na kwa bahati mbaya asilimia 90 ya
wananchi wake bado hawajapata huduma hii ya broadband majumbani mwao na
hivyo wako nyuma ukilinganisha na masoko yaliyoendelea.”
Huawei
walitumia mkutano huo pia kutambulisha mtandao wake wa LTE ambao
umepewa jina la “Mkakati wa Huawei kuelekea 5G”. Wakati wa utambulisho
huo, Huawei iliweka bayana mchakato mzima wa kuhama kutoka 3G kwenda
4G/4.5G hadi 5G.
Kuhamia
kwenye teknolojia ya LTE ni kuongeza ushindani. Teknolojia ya LTE
inazidi kukomaa baada ya teknolojia hiyo kusambaa kwenye mitandao.
Akitambulisha mtandao mpya wa 5G wakati wa warsha ya ‘Connect to Connet’
(C2C) ambayo pia ilidhaminiwa vilivyo na kampuni ya Huawei Tanzania,
Makamu wa Rais wa Huawei ‘Wireless marketing’, Alex Wang alisema “Huawei
wamesaidia ujenzi wa mitandao karibia 200 ya LTE dunia nzima na
kujizolea uzoefu wakutosha katika mageuzi ya mitandao ya simu.
Huawei
inaendelea kuwa makini katika kulinda uwekezaji wa wateja wake na
muhimu zaidi kulenga katika ukuaji na mageuzi ya mitandao ili kusaidia
wateja wake kuongeza ushindani”.
Mchango
wa Huawei katika utafiti wa 5G umetambulika katika sekta nzima na ndio
maana wakatunukiwa tuzo ya “Mchango bora katika maendeleo ya 5G” katika
warsha ya LTE iliyofanyika Amsterdam, Uholanzi wakati wa mkutano wa
dunia wa 5G tarehe 26 June 2015.
Hii
pia ni mara ya pili kwa serikali ya Tanzania kutambua mchango na
jitihada za Huawei nchini ambapo licha ya tuzo ya jana ni pamoja na
Huawei kutimiza makubaliano ya mkataba kati yake na serikali juu ya
mchakato wa teknolojia na mawasiliano ili kutimiza malengo ya nchi
ifikapo mwaka 2025.