Flatnews

Rais wa Ujerumani kuwasili Jumatatu

Joachim Gauck, Rais wa Ujerumani. Rais wa Ujerumani Joachim Gauck anawa...



Joachim Gauck, Rais wa Ujerumani.
Joachim Gauck, Rais wa Ujerumani.
Rais wa Ujerumani Joachim Gauck anawasili Jumatatu jioni kwa ziara ya siku tano.

Akiwa nchini Rais Gauck atakutana na Rais Kikwete, wabunge na wawakilishi wa mashirika ya kijami. Msafara wa Rais Gauck pia utajumuisha wafanya biashara wakubwa kutoka Ujerumani.
Tarehe 4 Rais Gauck ataelekea Zanzibar ambako atakutana na Rais Shein na baadae kuelekea Arusha. Akiwa mjini Arusha Joachim atatembelea mahakama ya Afrika ya Haki za binadamu, Makao makuu ya Afrika Mashariki na kuhutubia Bunge la Afrika Mashariki.
Akiwa Arusha Joachim pia atakabidhi Kituo cha Uendeshaji wa mapambano dhidi ya Ujangili kilichooko Seronera kwenye mbuga ya Serengeti na kilichoanzishwa na Shirika la Kisayansi za wanyama cha Ujerumani cha Deutsche Zoologische Gesellschaft.
Rais Gauck ataondoka nchini kurejea Ujerumani  Februari 6, akipitia Uwanja wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA).
Mkuu wa Serikali ya Ujerumani ni Chancelor, ingawa nchi hiyo pia ina Rais. Tofauti na nchi nyingine zenye mfumo kama huo ambako cheo hicho kinakuwa cha heshima tu, Rais wa Ujerumani ana madaraka kiasi fulani yakiwemo kuingia Mikataba ya Kimataifa kwa niaba ya nchi yake.

Related

H/KIMATAIFA 4088981011501610094

Post a Comment

emo-but-icon

item