Flatnews

PICHA: SUAREZ AIFANYIA MBAYA MAN CITY KATIKA UEFA

  Luis Suarez  Mshambuliaji wa Zamani wa Liverpool Luis Suarez amerejea nchini England hapo jana na bahati ya kipekee baada ya kuiwezes...



 
Luis Suarez 
Mshambuliaji wa Zamani wa Liverpool Luis Suarez amerejea nchini England hapo jana na bahati ya kipekee baada ya kuiwezesha timu yake mpya ya Barcelona kuibuka na ushindi wa mabao mawili 2 kwa moja dhidi ya wapinzani wao Manchester City katika mechi ya Klabu Bingwa barani Ulaya .

Luis Suárez of FC Barcelona celebrates after scoring their second goal during their UEFA Champions League round of 16 first leg against Manchester City FC
Javier Mascherano of FC Barcelona in action with Sergio Agüero (R) of Manchester City FC during their UEFA Champions League round of 16 first leg
 
Gaël Clichy of Manchester City FC in action with Ivan Rakitić (R) of FC Barcelona during their UEFA Champions League round of 16 first leg
  Sergio Agüero (R) of Manchester City FC looks dejected during their UEFA Champions League round of 16 first leg against FC Barcelona
Luis Suárez of FC Barcelona celebrates after scoring their second goal during their UEFA Champions League round of 16 first leg against Manchester City FC
 
Suarez aliwashangaza mashabiki wa Man City baada kupachika wavuni mabao yote mawili na hivyo kuwaonyesha ni moto wa kuotea mbali anapofika kwenye kisanduku cha kumi nane.
Goli pekee la kufutia machozi la Manchester City lilitiwa kimiani na mshambuliaji wa timu hiyo Sergio Aguero. Na hivyo hadi mechi hiyo inamalizikia Man City wakiwa nyumbani walijikuta wakivuna juani goli moja dhidi ya magoli mawali ya Barcelona.
Na katika mechi nyingine ya michuano hiyo Juventus ya Italia wakiwa nyumbani waliwaadhibu Borussia Dortmund ya Ujerumani baada ya kuwashushia kichapo cha magoli mawili kwa moja.
Magoli ya Juventus yalitiwa kimiani na Carlos Tevez na Alvaro Morata huku lile la Borussia Dortmund likitiwa kimiani na Marco Reus.
Kindumbwe ndumbe cha michuano hiyo kitaendelea tena hii leo ambapo Arsenal ya England watakuwa na kibarua kigumu dhidi ya Monaco ya Ufaransa huku Bayern Levekuzen wakimenyana vikali na Altetico Madrid ya Hispania. Mechi hizo zote zitapigwa mwendo wa saa 4:45 kwa saa za Afrika Mashariki.

Related

Suarez 6364520490855478558

Post a Comment

emo-but-icon

item