Maafisa Polisi 20 wauawa Afghanistan
Wanamgambo wa Taliban wamekuwa wakihatarisha usalama wa Afghanistan Maafisa Mashariki mwa Afghanista...
https://samchardtz.blogspot.com/2015/02/maafisa-polisi-20-wauawa-afghanistan.html
Maafisa
Mashariki mwa Afghanistan wamesema maafisa wa Polisi 20 wameuawa katika
mashambulio kadhaa.Watu wanne wameripotiwa kuvalia mavazi ya Polisi na
kuingia katika Ofisi za makao makuu ya Polisi katika jimbo la Logar, na
kujilipua.Gavana wa Jimbo hilo Niaz Muhammad Amiri ameiambia BBC kuwa Maafisa wengine wanane walijeruhiwa.Wengi kati ya waliopoteza maisha walikuwa wakipata chakuwa wakati wa mapumziko.
Kumekuwa na ongezeko la mashambulizi ya Wanamgambo miezi ya hivi karibuni wakati ambapo vikosi vya usalama vikiwa vimechukua udhibiti wa nchi hiyo kutoka kwa Majeshi ya NATO.